Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Erasmus Rugarabamu akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku sita ya Walimu Wakuu Shule za Msingi na Waratibu Elimu Kata juu ya muongozo wa uendeshaji wa shule (School Management Tool Kit) pamoja na usimamizi wa ufundishaji wa kusoma, kuandika na kuhesabu leo tarehe 03 Julai 2015. Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Serikali kupitia Wizara ya Elimu yanafanyika Mkoani Rukwa katika Chuo cha Ualimu Sumbawanga ambapo jumla ya washirikia 200 kutoka Halmashauri mbili za Manispaa ya Sumbawanga na Sumbawanga Vijijini wameshiriki kwenye awamu hii ya kwanza ya mafunzo. Mafunzo haya ni sehemu ya mpango wa BRN wenye lengo la kuinua ubora wa elimu nchini.
 Ndugu Nicholaus Moshi ambae ni Mratibu wa Programu ya Mafunzo ya Waalimu Kazini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi akizungumza katika Semina hiyo. Ndugu Moshi ni mmoja ya wawezeshaji wakuu katika Mafunzo hayo.
 Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...