THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.

  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com






MIONDOKO YA KUMEREMETA KWENYE MNUSO


Mkataa kwao mtumwa

Wssukuma na Nyoka wao...Mambo ya Bujora haya


NGOMA AZIPENDAZO ANKAL

Said Karoli hatosahaulika kwa ngoma yake ya 'Maria Salome'


JK awasili Addis Ababa kuhudhuria sherehe za miaka 50 za umoja wa nchi za afrika (AU)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ni miongomi mwa marais wa bara la Afrika watakaohudhuria Sherehe za kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazo fanyika rasmi leo Jumamosi Mei 25, 2013 katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia. 

 Shamrashamra zimetawala kila pembe ya jiji la Addis, wakati viongozi wa nchi za Afrika wakiwasili mmoja baada ya mwingine katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bole. 

 Muungano wa Afrika wakati huo ukijulikana kama OAU, ulizaliwa Mnamo Mei 25, 1963 jijini Addis Ababa, ukianza na nchi za 32 na baadaye nchi 21 zikajiunga miaka ilivyozidi kwenda, huku Afrika ya kusini ikijiunga kuwa mwanachama wa 53 mwaka 1994. 

Mwaka 2001 OAU iligeuzwa kuwa AU katika mkutano uliofanyika Lusaka, Zambia. Jumamosi hii kutakuwa na sherehe za kilele kuadhimisha miaka hiyo 50 ya AU na kuhudhuriwa na marais karibia wote wa Afrika. 

 Kauli mbiu ya sherehe za hapo kesho ni mjadala mkuu kuhusu ushirikiano wa nchi za Afrika na kuimarishwa kwa muungano huo. Mwenyekiti wa tume ya muungano huo, Dr Nkosazana Dlamini Zuma, anaseme kuwa hii itakuwa fursa kwa AU kujadili kuhusu uwezo wa bara hili na ambacho kinaweza kufikiwa katika miaka 50 ijayo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa alipowasili Ijumaa usiku  tayari kujiunga na viongozi wenzie wa nchi za Afrika katika sherehe za miaka 50  tangu kuanzishwa kwa Umoja  wa  nchi za Afrika (AU) zinazofanyika leo katika makao makuu ya umoja huo
Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete wakiwasili Addis Ababa
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakipata maelezo ya maandalizi ya sherehe hizo toka kwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Profesa Joram Biswaro mara baada ya kuwasili Addis Ababa


May 2013 Night Skies Over Tanzania


Wabunge wanawake wajinoa kuhusu namna bora ya uwasilishaji wa Miswada na Hoja Binafisi Bungeni

Chama cha Wabunge wanawake katika Bunge la Tanzania (TWGP) leo wamefanya semina ya siku moja kwa wabunge wote wanawake kwa lengo la kuongeza uelewa mpana katika namna bora ya uwasilishaji Miswada au hoja binafsi Bungeni.

Akifungua semina hiyo, Mwenyekiti wa chama hicho cha Wabunge wanawake Bungeni. Mhe. Anna Abdallah amewataka wabunge wanawake wote bila kujali vyama vyao kuhakikisha wanaitumia vizuri Ofisi ya mshauri mkuu wa mambo ya sheria wa Bunge katika kuwasilisha Miswada au hoja Binafisi.

Amesema wabunge wanawake wanawajibu wa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi hususani wanawake nchini ikiwa ni pamoja na kuleta hoja au miswada Bungeni yenye kulenga kuifanya serikali iweze kutatua kero zinazowakabili wananchi wake.

“Waheshimiwa wabunge, pamoja na kwamba mimi nikipindi changu cha nane hivi sasa bado kuna mwamko mdogo kwa waheshimiwa wabunge wanawake kuleta miswada au hoja binafsi bungeni. Naamini tukiitumia vizuri Ofisi hii pale tutakapokuwa tuna mawazo yetu, watatusaidia sana kutuandalia hoja binafisi au miswada kulingana na matakwa yaliyopo ya kikanuni”alisema Mhe. Anna Abdallah

wakichangia mada zilizowasilishwa hapo, wabunge wengi wanawake wameomba kuwe na utaratibu mzuri wa kuhakikisha kuwa kila mara elimu hii inatolewa kwa lengo la kujikumbusha baadhi ya taratibu za kikanuni na hata kisheria katika uwasilishaji wa hoja binafsi na miswada binafsi Bungeni.

“Kuna haja ya kuwa na semina katika maswala haya angalau mara moja kila wakati wa vikao vya Bunge ili kujikumbusha mambo kadhaa yanayotawala katika uwasilishwaji wa miswada binafsi au hoja Binafsi mwenyekiti kwa kuwa tuna mambo mengi tungependa kuyaleta Bungeni kupata baraka zake. Kwa kujikumbusha na mambo haya tutaiva kwelikweli katika kuwawakilisha wananchi wetu mwenyekiti”. Alichangia Mhe. Anne Kilango Malecela.

Jumla ya mada tatu ziliwasilishwa katika Semina hiyo iliyoandaliwa na chama hicho cha wabunge wanawake Bungeni (TWGP) kwa kushirikiana na Ofisi ya msahuri wa maswala ya sheria wa Bunge ambazo zote zililenga kuwapa uelewa wabunge kuhusu namna bora na mambo ya kuzingatia wakati wa kuwasilisha miswada binafsi na hoja binafsi Bungeni kwa wabunge wanawake.
Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge wanawake Bungeni (TWGP) . Mhe. Anna Abdallah (Mb) akifungua rasmi semina hiyo siku moja kuhusu namna bora ya uwasilishaji wa Miswada binafsi na hoja Binafisi Bungeni kwa wabunge wanawake. Kushoto ni katibu wa chama hicho Mhe. Angela kairuki na aliyekulia ni Makamu Mwenyekiti Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa.


adha ya foleni jijini dar


Dkt. Shein amtembelea Sheha Aliyetiwa Tindi kali huko Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) aliyemwagiwa Tindikali na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa pili kulia Kaka yake Sheha Sudu Mgeni Saidi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimuangalia Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) jinsi alivyoathirika na Tindikali alilomwagiwa na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa kushoto Dk.Slim Mohamed Mgeni,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]


Ujumbe TPA watembelea ubalozi wa Tanzania, Kigali

Pichani katikati mwenye Kaunda suti ni Col. Mrangila, kwa sasa ndio Mkuu wa Ubalozi, aliyeshikilia koti ni Magesa, Mkuu wa msafara wa TPA, wa kwanza kushoto ni Mwasswe Mwambata Msaidizi wa Kijeshi na wa mwisho kulia ni Mchani Mwambata wa kiuchumi, wengine pichani ni maafisa wakuu vitengo vya TPA idara za TEHAMA na Mipango. Maafisa wa Bandari wako Rwanda kubadilishana ujuzi namna ya kurahisisha biashara kwa kutumia Teknolojia ya Habari na MAwasiliano (TEHAMA), pia walitembelea wadau wa biashara Rwanda Kama Mamlaka ya Mapato Rwanda, Shirika la Viwango Rwanda, Chama Cha Mawakala wa Mizigo Rwanda n.k. Hivi karibuni Tanzania itaanza kutumia mfumo wa kufanya biashara kielectroniki kupitia Bandari na maeneo yote ya kuingia na Kutoka nje. Wadau kuweni Tayari....!!!!


WATAALAM WA TIBA ZA ASILI NA TIBA MBADALA WAKUTANA JIJINI DAR ES SALAAM

Kaimu mganga mkuu wa serikali Dkt. Mohamed Mohamed akifungua mkutano wa Baraza la wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala leo jijini Dar es salaam waliokutana kujadili mafanikio, changamoto na mipango mbalimbali waliyonayo katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Tiba za Asili na Tiba Mbadala wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt.Paulo Mohammed akitoa ufafanuzi wa hali halisi ya Tiba za Asili na Tiba mbadala nchini Tanzania na mpango wa serikali wa kuendelea kuthamini huduma inayotolewa na wataalam hao wakati wa mkutano wa Baraza la wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala.
Mratibu wa Tiba za Asili na Tiba Mbadala kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Rose Shija akisoma salam za mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatora leo jijini Dar es salaam ambaye amepongeza juhudi zinazofanywa na serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya kutatua changamoto zinazowakabili wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala.
Mtafiti mwandamizi mkuu wa Idara ya Utafiti wa Tiba Asili kutoka Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya Binadamu Hamis Masanja Malebo akitoa mada kuhusu historia ya Tiba za Asili na uhusiano uliopo katika matumizi ya mimea ya asili kati ya tiba za asili na tiba mbadala na tiba za kisasa katika utengenezaji wa dawa. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.
Sehemu ya wataalam wa Tiba za Asili na Tiba mbadala waliohudhuria mkutano wa Baraza la Wataalam wa tiba hiyo wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa mkutano huo leo jijini Dar es salaam. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.


TANZIA

MAREHEMU NDG. ERNEST ZULU
(1957 – 2013)
Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah, anasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wa Bunge, ndg. Ernest Zulu, Afisa Habari Mkuu, aliyefariki dunia tarehe 23/05/2013 akiwa masomoni nchini Malaysia, kwa maradhi ya kichwa yaliyomsumbua kwa muda mrefu.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kuja Tanzania kwa mazishi inaendelea. 

Taarifa ya ratiba kamili ya maziko itatolewa pindi mipango hiyo itakapokamilika. Ndg. Ernest Zulu alizaliwa tarehe 10 Julai, 1957 Songea Ruvuma na alipata Elimu ya uandishi wa Habari katika chuo cha Uandishi wa Habari cha TSJ (siku hizi SJMC) Jijini Dar es salaam na baadae kuajiriwa na shirika la Utangazaji la Tanzania (RTD) mwaka 1976 kama mwandishi wa Habari Msaidizi na hatimae kupandishwa cheo na kuwa Mwandishi wa Habari kabla ya kuhamia shirika la magazeti ya Chama la Uhuru na Mzalendo kama  Mwandishi Mwandamizi mwaka 1985, ambapo mwaka 1986 hadi 1987 alipata fursa ya kusomea masomo ya Uandishi wa Habari za Kimataifa huko nchini Urusi.

Mwaka 1991 aliajiriwa kama Mhariri Msaidizi katika gazeti la The Express kabla ya kujiunga na Sauti ya Ujerumani ambako alifanya kazi kama Mwandishi Mwandamizi kuanzia mwaka 1995.

Mwaka 1998 aliajiriwa na Ofisi ya Bunge kwa Cheo cha Afisa Habari Mwandamizi ambapo mpaka mauti inamkuta alikuwa Afisa Habari Mkuu daraja la pili.

Ndg. zulu alikwenda masomoni nchini Malaysia Julai, 2010 katika chuo kikuu cha Taylor akichukua Shahada ya kwanza ya Mawasiliano na usimamizi wa vyombo vya habari ambapo alitarajiwa kumaliza masomo yake mwaka huu Julai.

Marehemu ameacha Mjane na watoto Wanne.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya Marehemu mahala pema Peponi. Amina!

Imetolewa na Idara ya Habari,
Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
Ofisi ya Bunge
DODOMA

24 Mei, 2013


MBWA WALIOPATA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA UHALIFU

Mbwa wa kiraia aliyepatiwa mafunzo na Jeshi la Polisi ya namna ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu wanaobeba madawa ya kulevya hususani bangi.
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Mbwa akionyesha umahiri wake wa kutumia mnyama huyo mara baada ya kupatiwa mafunzo ya kutumia mbwa Kwa ajili ya kuzuia uhalifu na kikiosi cha mbwa na farasi cha Jeshi la Polisi mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam.
Mbwa akionyesha umahiri wake wa kumkamata muharifu.
Mmoja wa wahitimu wa kike aliyepata mafunzo ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi alipata mafunzo ya ukakamavu kwa ajili ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu, mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam katika viwanja vya kikosi cha mbwa na farasi cha jeshi la Polisi.( Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi).


American People Sponsor New Reproductive and Child Health Center at Lugalo

Commanding General of the United States Medical Research and Materiel Command, Brigadier General Joseph Caravalho (centre) being briefed by the Chief Medical Officer of the Tanzania People's Defense Force (TPDF) Reproductive and Child Health (RCH) Centre at Lugalo Military Hospital Colonel Juma Mwinula (Second from left) about a new operation theatre at the centre, after Brigadier General Caravalho inaugurated and handed over to TPDF the modern facility sponsored by the American People on May 24th, 2013. The modern center represents another milestone in the District of Mwenge, providing free mother and child health services including Prevention-of Mother-to-Child-Transmission (PMTCT), Anti-Retroviral Therapy (ART), and HIV testing and counseling services to more than 100,000 civilian and military residents. Right is TPDF's Major General Hassan Vuai Chema who represented the TPDF Chief of Defense Forces General Davis Mwamunyange at the event.


The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project Conducted a one day workshop to Mps and Staff on Social and Economic Policies

Yesterday the Office of the National Assembly and the UNDP under the Legislative Support Project organized a one day workshop on Social and economic Policies, Economic growth and development to the Members of the National Assembly and staff aiming at building capacity for Mps and Staff during the Budget session in Dodoma. The workshop is part of the Legislative Support Project to strengthen the capacity of the Mps and Staff in various areas for an effective Oversight, Legislation and representation.
One of the Presenter at the workshop on Social and economic Policies, Economic growth and development to the Members of the National Assembly Dr. Haji Semboja from the University of Dar es Salaam, presenting a topic on importance of social economic policies in the budget process for sustainable economic growth and development. The workshop was organized by the office of The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project.
Hon. Madabida giving her contribution to the presenters.
Hon. Suleman Zedi curiously posing a question to the presenter during the workshop.


Niyonzima asaini mkataba wa miaka 2 Yanga

HATIMAYE uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Tanzania bara Yanga leo imempa mkataba wa miaka miwili kiungo wake mchezeshaji Haruna Niyonzima huku kukiwa na taarifa kuwa kiungo huyo amemwaga wino kwa dau la dola 70,000 sawa na Shilingi 111,654,000 milioni sambamba na mshahara wa dola 3,000 ingawa Yanga wenyewe wamegoma kuweka wazi kiasi hicho cha fedha.

Mshahara huo wa Niyonzima umepanda baada ya awali kupokea dola 1500 na kusajiliwa kwake, kumezikata ngebe klabu ambazo zilikuwa zikimnyemelea wakiwemo wapinzani wao Simba sambamba na Azam ikiwa ni pamoja na klabu moja ya nchini Tunisia.

Akizungumza Makao Mkuu ya klabu hiyo Niyonzima ambaye pia aliangusha chozi baada ya kukumbushwa baba yake mzazi aliyefariki miaka mingi alisema "Watu walitaka kujua mimi nitaenda wapi, ninachotaka kusema kwa sasa nimeamua kusaini Yanga na nitaitumikia kwa nguvu zangu zote kwa miaka miwili, na kwa sasa akili yangu naelekeza Kombe la Kagame.

"Kama wachezaji tumekuwa na matatizo mengi, ni kweli timu nyingi zilinifuata lakini niliamua kutuliza kichwa kwanza kabla sijaamua kufanya chochote, naheshimu kazi yangu, na ningependa Mungu anijalie hata nikimaliza mkataba huu mpya niendelee kuichezea Yanga."alisema Mnyarwanda huyo ambaye msimu uliopita alipata ulaji kwenda kuichezea timu ya El Merreikh ya Sudan na klabu hiyo ya Jangwani ilimzuia.

Hata hivyo habari ambazo zilizipatikana jana zinasema kuwa katika kikao kilichofanyika juzi jioni makao makuu ya klabu hiyo kulikuwa na mvutano mkubwa wa viongozi ambao wengine walitaka waachane na kiungo huyo ambaye alikuwa akiwadengulia kumwaga wino akitaka donge nono zaidi, wakifananisha na Sunday Manara 'Computer' ambaye alishawai kuitosa timu hiyo na kwenda Pan Afrika wakati akiwa ni mchezaji tegemeo.

Lakini jana Katibu mkuu wa klabu hiyo Laurance Mwalusako alisema wameamua kumuongezea mkataba Niyonzia kufuatia klabu hiyo kuhitaji mchango wake hasa katika michuano yao ya kimataifa kwani katika kipindi cha miaka miwili ameonyesha kiwango cha hali ya juu.

"Yamekuwa yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.

Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.


Korogwe yatia fora mapokezi mwenge wa uhuru

Na Mashaka Mhando,Korogwe 

WILAYA ya Korogwe mkoani Tanga, imetia fora katika mbio za Mwenge wa Uhuru uliomaliza mbio zake mkoani hapa jana, kwa kuwapanga wananchi kuulaki mwenge huo kila ulipokuwa ukipita katika vijiji mbalimbali.

Mwenge huo uliopokelewa katika Kijiji cha Makole kilichopo kata ya Magamba-Kwalukonge kutokea wilaya ya Kilindi, Mkuu wa wilaya hiyo Mrisho Gambo mara baada ya kuupokea mwenge huo, alisema kwamba utakimbizwa na kufungua miradi saba yenye jumla ya sh. 1,392,142,300.

Akizungumza katika mikutano mbalimbali katika kutoa ujumbe wa mwenge mwaka huu, kiongozi wa mwenge huo Juma Ali Simai, alirejea kauli yake ya kuwataka Watanzania kuepuka migogoro inayoweza kuwagawa na kuvunjika kwa amani.

Alisema baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alitumia baiskeli wakati akihamasisha wananchi kudai uhuru na maara baada ya kupata alijenga misingi ya umoja, mshikamano na upendo miongoni mwa Watanzania.

Hivyo, watu wanaochezea amani kwa kutaka kuwagawa wanafanya makosa makubwa ni vema wananchi wakaacha kuwaunga mkono kwani wapo wananchi wan chi nyingine wamekuwa hawatembei nyakati za mchana na usiku kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

“Wapo wenzetu wengine katika nchi zao hawatembei kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe, hawa wanajiuliza hivi Tanzania wamefanya nini hadi leo wana amani…Jamani hii amani tuilinde tuache kubaguana kwa misingi ya dini, rasilimali tuendeleze mshikamano tuliokuwa nao,” alisema Simai.


Akizungumza katika mkesha wa mwenge katika kijiji cha Kwashemshi, mbunge wa jimbo la Korogwe Vijijini Stephen Ngonyani ‘almaarufu Profesa Majimarefu’, alisema wilaya hiyo bado imekuwa na mshikamano miongoni mwa wananchi kiasi kwamba, wanatumia nafasi hiyo kufanya kazi za maendeleo katika vijiji vyao.


Mkesha huo uliombatana na watu kupima VVU na Ukimwi pamoja na watu mbalimbali kujitokeza kutoa damu kwa hiari katika zoezi ambalo pia Mwandishi wa habari hizi Bw. Mashaka Mhando, alitoa damu kiasi cya unit moja kati ya unit 50 zilizopatikana.

Mhando alisema ameaamua kutoa damu kwasababu wilaya ya Korogwe katika hospitali ya magunga huwa majeruhi wengi wamekuwa wakipata shida kubwa ya kuongezewa damu hivyo uhamasishaji wao wa kutoa damu salama unatakiwa kuungwa mkono.

Mwenge umamaliza mbio zake mkoani Tanga na leo umeanza mbio zake mkoani Kilimanjaro kwa kuanzia wilaya ya Same.


MCHOCHEZI WA VURUGU NA FUJO NCHINI AKAMATWA

Jeshi la Polisi Nchini linamshikilia mtu mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi kwa tuhuma za kueneza ujumbe wa uchochezi na chuki kwa wananchi na viongozi wa serikali kwa njia ya simu ya mkononi akituma SMS kwa lengo la kuchochea fujo, vurugu na kutoa matusi kwa viongozi hao.

Mtu huyo amekuwa akifanikisha kazi hiyo kwa kutumia Chips (sim card) 13 za simu za mkononi ambazo amekamatwa nazo. Jeshi la Polisi linaendelea kumhoji mtu huyo na ushahidi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

Aidha, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wenye taarifa zingine za wahahlifu kama hao kujitokeza na kutoa taarifa hizo polisi ili wahalifu hao waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua stahiki, wakiwemo watu wanaowashawishi wenzao kwa njia ya fedha, kuwashauri ama kuwasaidia kwa namna yeyote ile katika kufanikisha uhalifu huo na kusababisha uvunjifu wa amani hapa nchini. Jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kuvunja sheria za nchi.

Imetolewa na:-
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.


RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA MAONYESHO YA MFUMO WA MATOKEO MAKUBWA 'SASA' AWAMU YA KWANZA

Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya kwanza.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mchambuzi Sera Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mipango, Lorah Madete, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtafiti Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Shetto, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwa kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wakati wa Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya Kwanza leo Mei 24, 2013.
Wanamuziki wa Bendi ya Mjomba, wakiimba kutoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa 'Sasa' Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR

BOFYA HAPA KUSOKA HOTUBA YA RAIS


Benki ya Stanbic Tanzania yazidi kuboresha huduma zake.

 Mkurugenzi mkuu wa Stanbic Bank,Bwa Bashir Awale akimkabidhi zawadi ya heshima mgeni rasmi,Mwenyekiti wa kampuni ya ndege ya Precision Air,Bwa.Michael Shirima kwenye hafla ya benki hiyo iliyohusu maboresho zaidi katika huduma yake ya kibenki itolewayo kwa wateja wenye mahitaji maalum (Executive Banking), kwa lengo la kuwaondolea usumbufu, kuwapa huduma kwa kulingana na mahitaji yao maalum, kuhudumiwa kwa wakati wanaotaka wao na kuwapa faida zaidi.
Pichani ni Mgeni rasmi,Mwenyekiti wa kampuni ya ndege ya Precision Air,Bwa.Michael Shirima akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla ya Stanbic Bank iliyohusu maboresho zaidi katika huduma yake ya kibenki itolewayo kwa wateja wenye mahitaji maalum (Executive Banking), kwa lengo la kuwaondolea usumbufu, kuwapa huduma kwa kulingana na mahitaji yao maalum, kuhudumiwa kwa wakati wanaotaka wao na kuwapa faida zaidi.Hafla hiyo imefanyika leo jioni ,ndani ya hotel ya Hyatt kempinsk jijini Dar.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano katika Benki ya Stanbic  Tanzania,Bwa.Abdallah Singano akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla ya Stanbic Bank iliyohusu maboresho zaidi katika huduma yake ya kibenki itolewayo kwa wateja wenye mahitaji maalum (Executive Banking product), kwa lengo la kuwaondolea usumbufu, kuwapa huduma kwa kulingana na mahitaji yao maalum, kuhudumiwa kwa wakati wanaotaka wao na kuwapa faida zaidi.Hafla hiyo imefanyika leo jioni ,ndani ya hotel ya Hyatt kempinsk jijini Dar.

Bwa.Singano alisema kuwa Wateja wa benki hiyo sasa wataepuka ulipaji wa ada mbali mbali na zisizotabirika, na hivyo kwa ada ya kila mwezi au kiasi kidogo cha akiba katika akaunti, mteja atahakikishiwa kupata faida nyingi na huduma bora kwa wakati wake. 
Mkuu wa Kitengo cha huduma za kibenki binafsi na za kibiashara, Paul Omara akizungumza wakati wa hafla ya kukuza mahusiano baina ya wafanyakazi wa benki hiyo na wateja, iliyofanyika  jioni ya leo katika hoteli ya Hyatt jijini Dar es Salaam, alisema kuwa huduma hiyo imesukwa upya na kuundwa kutokana na marejesho ya wateja ya jinsi gani wanahitaji wahudumiwe na maoni yao juu ya uboreshaji wa huduma za benki hiyo kwa ujumla.


kutoka bungeni dodoma leo

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mh Samuel Sitta akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2013/14 Bungeni mjini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria,Mh Mathias Chikawe (kushoto), Mbunge wa Sengerema,Mh William Ngeleja na Mbunge wa Peramio, Mh Jenister Mhagama wakifurahi jambo wakati wakitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana. Picha zote na Zawadi Msalla wa MAELEZO.


Segera ya sasa ionekanavyo

 Hiki ni kipita shoto kilichopo kwenye makutano ya barabara ya Tanga,Moshi na Dar es Salaam kilichopo Segera.hivi ndivyo kionekanavyo sasa baada ya kukamilika matengenezo yake.
Hiki ni kituo cha Mabasi mbali mbali yapitayo katika eneo hilo la Segera Mkoani Tanga.


Forbes winner Patrick Ngowi embraces Obama’s Energy plan for Africa


By Amani Nkurlu

Obama’s intention to unveil Africa’s Power Supply Plan while in Tanzania will be of great significance to the country and the continent at large say’s Forbes 30 under 30 – Africa’s Best Young Entrepreneurs Award winner Patrick Ngowi.

Commenting on confirmed reports that the US President will be visiting sub-saharan Africa next month, Engineer Patrick Ngowi (28), who is also the Managing Director & CEO for Helvetic Solar Contractors said that the energy plan which will be historically announced in Tanzania should be whole heartedly embraced, as it is very meaningful for development of people and the country’s economy.

“Energy plays a very crucial role when it comes to the progress of any country. Therefore, Tanzania and Africa at large are not excluded when looking for viable solutions towards our power woes. I am confident that in partnership with the United States, we can make a valuable contribution to this,” he said.

According to Eng. Ngowi, when he learnt that only 14 percent of Tanzania has access to electricity that’s when he decided to venture into the Solar business and is now making a difference to the Tanzanian community through renewable energy. “I did not only see a problem, but an opportunity, which I applied a feasible solution to. And here I am today, promoting young entrepreneurship through renewable energy,” he added.

Apart from listing on Forbes 2013: ‘30 under 30’ Africa Award, the young entrepreneur has also managed to bag the Fastest Growing and Number One spot in the Top 100 Mid Sized Company in Tanzania 2012 - 2013 survey conducted by The Citizen, Mwananchi Communications, NBC Bank and KPMG (East Africa).

Eng. Ngowi -- founder of Helvetic Solar Contractors supplies, installs and maintains all types of solar power and thermal systems in Tanzania and across East Africa. Last year his company made about $3 million in revenues.


Balozi Seif Idd akuna na Balozi wa Norway Nchini pia awashukuru Madaktari Mabingwa wa China kwa mchango wao mkubwa

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Balozi wa Norway Nchini Tanzania Bibi Inguun Klepsvik Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar na kuiomba Norway kuangalia uwezekano wa kusaidia utaalamu wa Uvuvi wa Bahari Kuu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwashukuru Madaktari Mabingwa wa China kwa mchango wao mkubwa wa huduma bora za afya ndani ya kipindi chao cha miaka Miwili ambao wanatarajiwa kumaliza muda wao ifikapo mwezi ujao wa Juni mwaka huu.Hafla hiyo ya chakula cha usiku aliwaandalia hapo katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resor Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na Madaktari Mabingwa wa China wanaotoa huduma za afya katika Hospitali mbali mbali za Zanzibar mara baada ya kula nao chakula cha usiku alichowaandalia ikiwa ni ishara ya kuwaaga rasmi baada ya kumaliza muda wao wa miaka miwili hapa Zanzibar. Picha na Hassan Issa wa - OMPR – ZNZ.


MSEMO WA LEO KWENYE BODA BODA


MKALI WA VODACOM

Je, unajiamini kuwa na kitu kinachokufanya uwe mkali mtarajiwa? Vodacom inatafuta mtangazaji mpya wa kipindi cha TV kitakachoanza hivi karibuni. Soma namna ya kushiriki na unaweza kuwa mmoja ya watangazaji wa kipindi hiki.
Kazi ni kwako.


Nafasi za Kazi katika fani za ICT na IEC - wadau tuchangamke

IEC Communications Position 2 Job Description


MKALI WA VODACOM

Je, unajiamini kuwa na kitu kinachokufanya uwe mkali mtarajiwa? Vodacom inatafuta mtangazaji mpya wa kipindi cha TV kitakachoanza hivi karibuni. Soma namna ya kushiriki na unaweza kuwa mmoja ya watangazaji wa kipindi hiki. Kazi ni kwako.


Viongozi watakiwa kutatua ‘bomu’ la ajira kwa vijana

Katibu Mtendaji wa APRM Tanzania, Rehema Twalib akihudhuria Mkutano wa miaka 10 ya APRM na 50 ya AU mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Na Hassan Abbas, Addis Ababa

VIONGOZI wa Afrika wameshauriwa kuweka mikakati madhubuti ya kutatua tatizo la ajira kwa vijana ambalo limetajwa kuwa sawa na bomu linalosubiri kuripuka. Mpango wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) nao umeshauriwa kufanyiakazi suala hilo.

Changamoto hiyo imetolewa mjini hapa wakati wa mikutano ya kutafakari miaka 10 ya APRM na 50 ya Umoja wa Afrika (AU). Akichangia mada kuhusu utawala bora Barani Afrika, Wakili Maitre Tully kutoka Taasisi ya Kusikiliza Malalamiko ya Wananchi ya Afrika Kusini, alisema sehemu kubwa ya wakazi wa Afrika ya leo ni vijana.

“Takwimu zinaonesha Afrika ina vijana wengi zaidi kuliko sehemu yoyote duniani. Hata hivyo zaidi ya asilimia 60 ya vijana hao hawana ajira,” alisema, hoja iliyoungwa mkono na washiriki wengi wakiwemo wataalamu mbalimbali kutoka APRM.

Kwa upande wake mmoja wa wajumbe wa Jopo la Watu Mashuhuri la APRM, Balozi Fatma Ndagiza alitaka vijana wakumbukwe katika mipango ya maendeleo ikiwemo kupewa taarifa juu ya masuala muhimu yanayohusu nchi zao.

Balozi Fatma ambaye alipata kuwa Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, alisema vijana wakipewa taarifa kupitia mitandao ya kijamii watakuwa wamejengewa uwezo wa kujiamini na kushiriki katika maendeleo ya nchi zao.

Akieleza sababu za vijana wengi wa Afrika kukosa ajira, mtaalamu wa masuala ya elimu Prof. Mbaya Kankwenda, alisema elimu inayotolewa Barani Afrika imeshindwa kuzalisha watu “waliona ujuzi na taaluma” bali “wahitimu.”

“Leo Afrika vijana wanasomeshwa kwa kutumia rejea ya vitabu vya maprofesa wa Ulaya ambavyo hata huko Ulaya hakuna anayevisoma,” alisema.

Alisisitiza kuwa vijana wa Afrika sasa wanapewa elimu itakayowapa ujuzi na taaluma mbalimbali zitakazowasaidia kuwa wabunifu katika elimwengu wa sasa unaohitaji watu wenye ujuzi.

Naye Dr. Jean Butera kutoka Rwanda aliwagusa washiriki wengi aliposema kuwa elimu itolewayo sasa kwa vijana haitekelezi ajenda ya kuwasaidia vijana wa Afrika bali “ajenda isiyojulikana.”

“Elimu isiyofuata misingi ya maadili na mahitaji ya Afrika itaishia tu kuwapatia vyeti vijana wetu na si taaluma muhimu. APRM lazima iingilie katika katika eneo hili kwa kufanya utafiti na kuwashauri viongozi wa Afrika juu ya ni mitaala gani inayoweza kuwasaidia vijana wa Afrika kuliko ya sasa?” alitoa hoja.

Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa ni miongoni mwa watu ambao wamekuwa wakipigania kuwepo kwa mikakati nchini ya kusaidia kutatia tatizo linaloongezeka la vijana wengi kukosa ajira.


BTG WORKSHOP ON "LEADERSHIP SKILLS FOR GLOBAL MARKET

BTG Group LTD (www.btgforafrica.com) is holding a one-day workshop titled: Leadership Skills for the Global Marketplace. Attendees will receive training in: 

Business Negotiations 
Cultural Intelligence 
Leadership Values 
Cyber Security Management 

The quality of your business's employees is directly related to the success of your organization. The strategies and topics covered during this workshop will give your employees the edge in advancing your business. 

Date: Thursday 6, June 2013 
Time: 9AM - 4PM 
Location: Holiday Inn, Dar es Salaam, City Centre 

For registration and details, please visit: www.btgforafrica.com/workshop 

We hope to see you there! 


NSSF YAWAPOKEA WANACHAMA WAPYA WA HIARI 500 JIJINI TANGA

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza akiwasalimia wakazi wa Kata ya Kwale, Wilayani Mkinga ambapo zaidi ya Wananchi Mia Tano (500) wamejiunga na NSSF kama wanachama wa hiari.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF Bw. Crescentius Magori akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza na Meneja Wa NSSF mkoa wa Tanga Bw. Frank Maduga. Kulia kwake Ni Bi Eunice Chiume, Meneja Kiongozi wa Uhusiano na Uhuduma kwa Wateja.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kichalikani akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza hotuba ya wakazi wa Kata ya Kwale.
Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza akiwakabidhi wanachama wapya wa hiari wa NSSF katika Kata ya Kwale.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI