Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
KAMPUNI ya Utoaji Mikopo kwa Mabenki na Taasisi za fedha kwa ajili ya mikopo wa nyumba Tanzania (TMRC), imezindua mpango wa hatifungani wa miaka mitano kwenye Soko la Hisa (DSE).

Uzinduzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni hiyo Ammish Owusu-Amoah ameongoza uzinduzi huo ambao pia umeshuhudiwa na wawekezaji pamoja na wadau mbalimbali toka sekta za fedha, nyumba na sekta nyingine.

Hivyo uzinduzi wa utoaji wa dhamana ya TMRC ulifanyika baada ya TMRC kupokea kibali kwa ajili programu ya utoaji wa dhamana ya miaka 5 yenye thamani ya Sh. Bilioni 120. Mpango huo ulipata kibali kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Masoko ya Mitaji (CMSA) pamoja na Soko la Hisa (DSE). Kampuni hiyo ya TMRC itaorodheshwa kwenye DSE.

Aidha, CMSA na DSE, zilijumuisha kuendelea kwa TMRC kutoa dhamana ya ushirika wake ambayo itakuwa kiasi cha Sh Bilioni 12.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Utoaji Mikopo kwa Benki na Taasisi za fedha kwa ajili ya mikopo wa nyumba Tanzania (TMRC) Oscar Mgaya akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa NMB Plc, Ineke Bussemaker( wa tatu kutoka kulia) pamoja na Mwenyekiti wa TMRC ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya BOA Tanzania, Ammishaddai Owusu-Amoah, wakikata kwa pamoja utepe wa uzinduzi wa mpango wa hatifungan.
 Mtendaji Mkuu wa Fedha wa TMRC, Oswald Urassa akiwaelezwa wadau mambo mbalimbali kuhusu utekelezaji wa kampuni ya TMRC.
 Mwenyekiti wa kampuni ya TMRC, Ammishaddai Owusu-Amoah, akifafanua jambo wakati wa uzinduzi wa mpango wa hatifungani wa miaka mitano kwenye Soko la Hisa (DSE).
Baadhi ya wageni walioshiriki wakimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Utoaji Mikopo kwa Benki na Taasisi za fedha kwa ajili ya mikopo wa nyumba Tanzania (TMRC) Oscar Mgaya  kwenye uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...