Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (Mb) wakati akipokea mbio za mwenge wa Uhuru ulipowasili Wilaya ya Kibondo kwenye jimbo lake la Muhambwe ukitokea Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma. Amesema kuwa Wilaya ya Kibondo imeongoza kwa ufaulu wa shule za sekondari kwa miaka miwili mfululizo ya masomo mwaka 2016 na 2017 ambapo kidato cha pili wameshika nafasi ya nane kitaifa na kidato cha nne wameshika nafasi ya tisa kitaifa na kuzibwaga sekondari nyingine zilizopo kwenye jumla ya Wilaya 187 nchini.
Nditiye amefafanua kuwa shule hizo zimezawadiwa kiasi cha shilingi milioni 680 na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Mpango wa Elimu kwa Matokeo (E4P) ambao umeleta chachu, ari na ushindani kwenye kiwango cha ufaulu kwenye shule mbalimbali nchini. Amefafanua kuwa fedha hizo zimetumika kugharamia upatikanaji wa miundombinu mbalimbali kwenye shule ya sekondari ya Malagarasi na ya Wasichana ya Kibondo.
Ameongeza kuwa ushindi huo umeleta chachu na mwamko zaidi kwa wanafunzi, walimu, wazazi, walezi na wadau wa elimu kwenye Wilaya hiyo ambapo wamejipanga kuchangia ujenzi wa miundombinu mbali mbali kwenye shule za Wilaya hiyo ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi ambapo imeendana na kauli Mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu isemayo, “Elimu ni Ufunguo wa Maisha, Wekeza Sasa kwenye Elimu kwa Maendeleo ya Taifa”.
Mhandisi Nditiye amesema kuwa Wilaya ya Kibondo inaunga mkono jitihada za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muunano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli za kutoa elimu bure nchini kote kwa shule za msingi na sekondari ambapo wazazi hawalipi ada yeyote hivyo inawawezesha kushirikiana kuendeleza miundombinu ya shule na mahitaji ya huduma nyingine ili wanafunzi waweze kujisomea na hivyo kuongeza ufaulu wao.
Naibu
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (Mb)
akipokea Mwenge wa Uhuru baada ya kuwasili kwenye jimbo lake la Muhambwe
Wilayani Kibondo mkoani Kigoma.
Naibu
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa pili
kushoto) akishiriki uzinduzi wa Kituo cha Afya cha Mabamba kilichopo
kwenye jimbo lake la Muhambwe wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru za
kitaifa uliofanyiwa na kiongozi wa kitaifa wa mbio hizo Bwana Charles
Kabeho (wa tatu kushoto) kwenye kata ya Mabamba wilayani Kibondo, Kigoma
Mkuu
wa Wilaya ya Kibondo Mheshimiwa Loyce Bura (kulia) akipokea mbio za
Mwenge wa Uhuru wa Taifa kwenye kijiji cha Mkubwa kilichopo mpakani mwa
Wilaya ya Kibondo na Kakonko
Naibu
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akigawa
chandarua kwa wanawake wenye watoto baada ya uzinduzi wa kituo cha Afya
cha Mabamba kilichopo kwenye jimbo lake la Muhambwe wilayani Kibondo,
Kigoma wakati wa mbio za Mwenge wa uhuru za kitaifa
Naibu
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye, Mbunge wa
jimbo la Muhambwe wilayani Kibondo, Kigoma akipiga ngoma kuburudisha
wapiga kura wake wakati wa kupokea mbio za Mwenge wa Uhuru za kitaifa
uliowasili kwenye Wilaya hiyo
Shule
za sekondari za Wilaya ya Kibondo zaongoza kwa ufaulu wa elimu katika
ngazi ya kitaifa kwa miaka miwili mfululizo na kushika nafasi kati ya
shule kumi bora za kitaifa na kuzishinda wilaya nyingine zote nchini
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...