Upatikanaji wa maji mijini na vijijini umeimarika kutoka chini ya 50% ya awali kutokana na umakini katika ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji safi nchini. Aidha, ili kukabiliana na mazingira Serikali imeanza mchakato wa kutumia mifumo ya kisayansi ili kuondoa matumizi ya mkaa majumbani.

Hatua hizo zimebainishwa na Mhe. Isack Kamwelwe, Waziri wa Maji na Umwagiliaji na Mhe. Januari Makamba, Waziri wa Nchi (Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira) walipokuwa wakieleza utekelezaji wa hoja za CAG katika sekta zao.

Akizungumzia hoja kuhusu utekelezaji wa miradi ya maji nchini, Waziri Kamwelwe amesisitiza kuwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, ufuatiliaji na kuzibwa mianya ya ubadhirifu vimeleta mafanikio makubwa katika utekelezaji wa miradi ya maji mijini na vijijini.

“Sisi kwa upande wetu CAG anatuonesha njia ili tufanye vizuri zaidi. Hadi kufikia Desemba, 2017, upatikanaji wa maji mijini umepanda hadi kufikia asilimia 78. Kwa upande wa vijijini, hadi kufikia Machi 2018, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imejenga vituo vya kuchotea maji 123,888 vyenye uwezo wa kuhudumia takribani watu milioni 30 sawa na asilimia 68.8,” alisema.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe akijibu hoja mbalimbali zilizobainishwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  katika Wizara yake mapema mjini Dodoma  wakati wa mkutano na waandishi wa habari ( hawapo pichani).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January   Makamba akijibu hoja mbalimnbali zilizobainishwa katika ripoti  ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  katika Ofisi hiyo mapema mjini Dodoma wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani).
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akisisitiza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utaratibu wa Mawaziri wote kukutana na waandishi wa habari kujibu hoja mbalimbali zilizobainishwa katika  ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  katika Wizara zao mapema mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akifurahia jambo na Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa  Aweso  mapema mjini Dodoma wakati wa mkutano  na waandishi wa habari uliowashirikisha  Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January  Makamba. (Picha zote  na Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma)


 KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...