Na Atley Kuni OR TAMISEMI
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema kuanza kwa kozi za ngazi ya Shahada katika Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo kisiwe kigezo cha kuondosha kozi za Astashahada na Stashahada katika chuo hicho.
Waziri Jafo alikuwa akizundua rasmi Bustani ya  Magufuli katika chuo hicho ambapo Bustani hiyo itatumika kuishi na kuenzi mchango wa kiongozi huyo wa Nchi kwasasa ambao ni uzalendo, kujituma pamoja na uadilifu katika kuwatumikia wananchi.
“Nimesikia maombi yenu yakutaka Kuanzishwa kwa kozi za Ngazi ya Shahada kusudi mtu anapo hitimu masomo yake ya ngazi za awali aweze kuendelea, naomba niwambie, tutajitahidi lifanikiwe, lakini angalizo langu kwenu, tutakapo anzisha Degree isiwe sababu yakusitisha kozi zinazoendelea kwa sasa, ikiwepo Astashahada (Certificate) na Stashahada (Diploma) ya kozi mnazo endelea nazo” amesema Jafo.
Waziri Jafo amesema, vyuo vingi vilipo anzisha ngazi ya Shahada na kusahau wataalam wa kada za kati vilichochea kukosekana kwa wataalam wakutosha katika ngazi ya kati hususan mafundi mchundo ambao walikuwa wakizalishwa katika vyuo hivyo.
Katika hatua nyingine Waziri Jafo amewahakikishia Wakurufunzi hao wa chuo cha Hombolo uhakika wa kuajiriwa na Serikali kwa wale watakao fikia vigezo vinavyo hitajika katika nafasi mbali mbali ambazo serikali itatangaza.
 Waziri wa Nchi OR TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo (Mb), akizungumza  wakati wa uzunduzi wa mnara wa kuenzi uzalendo wa Mhe. Rais wa awamu ya tano wa Tanzania katika chuo cha Hombolo.




Baadhi ya watendaji wa Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo wakati wa zoezi la uzinduzi wa mnara wa fikra za kizalendo za Mhe. Rais Magufu
 Kikundi cha Ngoma za asili cha Swala kitoa borudani wakati wa  wa uzunduzi wa mnara wa kuenzi uzalendo wa Mhe. Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, kikundi hicho kinachopatikana katika Kijiji cha Nkoyo, Hombolo ambacho ni maarufu katika mkoa wa Dodoma hususani kudumisha utamaduni wa mtanzania.
Mwonekano wa Mnara wa Magufuli Square, Sehemu iliyojengwa mahususi kwa ajili ya kuenzi uzalendo wa Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa vitendo
 Bodi ya Chuo cha Hombolo iliyo maliza muda wake wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa mnara wa fikra za kizalendo za Mhe. Rais Magufuli.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...