Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

IDARA ya Uhamiaji nchini imefanya usafi katika Kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu na Shule ya Msingi ya Matumaini ya Jeshi la Waokovu ‘Salvation Army’ iliyopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza kufanya usafi katika shule hiyo,kwa niaba ya Kamishina Jenerali wa Idara hiyo , Kamishina wa Utawala na Fedha, Edward Chogera amesema tangu kutangzwa Siku ya Jumamosi ni ya kufanya usafi Idara yai imekuwa ikifanya jitihada za kufanya usafi huo katika maeneo ambayo yana mchango kwa jamii.

Amesema shule ya Matumaini na kituo ni sehemu muhimu kutokana na watoto wanaosoma hapo kuwa na mahitaji maalumu.Kituo hicho hakiwezi kufanya chenyewe kutokana na mazingira ya watoto hao.Ameongeza mbali ya kufanya usafi katika kituo hicho wametoa pia msaada wenye thamani sh.500,000 ambao umetokana na wafanyakazi wa idara na wadau wenye ni njema kusaidia kundi maalumu ya kituo cha Jeshi la Uokovu .

Aidha amesema katika kipindi kijacho wamepanga kuwafikia watu wengine katika kufanya usafi ikiwa ni sehemu ya wafanyakazi kujua jamii inayowazunguka.Msaada waliotoa ni , Mchele, Maharage sukari , Mafuta ya kula , Sabuni za kuogea , Unga wa mahindi na mafuta ya kupakaa kwa wanafunzi wenye Ualbino .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo hicho,Timoth Sinana amesema licha kupata elimu,watoto wamekuwa wamekuwa wakiendelezwa kwenye mambo mbalimbali yakiwamo ufundi nguo na kuendeleza vipaji vyao.Amesema wanafunzi hao wamekuwa bora kimkoa katika suala la vipaji.
Kamishina wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji , Edward Chogera akizungumza wanafunzi na walimu pamoja na walezi wa kituo na shule ya Matumaini ya Jeshi la Waokovu Salvation Army mara baada ya kumaliza usafi katika kituo hicho jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kituo cha Jeshi la Waokovu pamoja shule ya Matumaini, Timoth Sinana akizungumza kuhusiana na historia ya shule hiyo tangu ilipoanzishwa mwaka 1969 pamoja na mafanikio ya shule hiyo .
Msaada uliotolewa katika kituoa hicho ni , Mchele, Maharage sukari , Mafuta ya Kula , Sabuni za Kuogea , Unga wa Mahindi pamoja na mafuta ya kupakaa kwa wanafunzi Wenye Ualbino .  

Baadhi wa wafanyakazi katika shule ya msingi ya matumaini na kituo cha jeshi la Waokovu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...