Wananchi mkoani Mara wamejitokeza kwa wingi kutekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Kighoma Ali Malima ambaye amewataka wakazi wote wa mkoa huo kuhakikisha wanasajiliwa Vitambulisho vya Taifa ndani ya miezi mitatu ya zoezi hilo linaloendelea katika Wilaya zote za mkoa huo.
Akizungumzia mwitikio wa wananchi katika kutekeleza agizo hilo; Afisa Usajili Wilaya ya Musoma Bi. Ohana Gerald amesema mwitikio mkubwa wa watu ndiyo umepelekea kwa Wilaya ya Musoma Manispaa; zoezi la usajili kuwa  limekamilika na sasa zoezi linaendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Vijijini na tayari Kata za  Bwasi, Makojo na Bukumi zimemaliza Usajili. Kata zinazoendelea na usajili kwa sasa ni Bukima, Suguti na Rusoli.
Aidha amewataka wananchi wa kata nyingine 15 ambazo bado usajili haujaanza kuanza maandalizi na kujitokeza kwa wingi pindi zoezi litakapofika katika kata zao.
Baadhi ya wananchi wameonyesha uelewa mpana wa manufaa ya kuwa na Vitambulisho vya Taifa na kuishukuru Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kuendesha zoezi bila kulipia gharama zozote.
Pamoja na kuisifu Serikali wamemshukuru Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Malima kwa kuweka msukumo mkubwa wa zoezi la Usajili kwani kwa muda mrefu wananchi wamekuwa wakinyanyasika kwa kukosa utambulisho na hivyo kukosa fursa nyingi na kuwapunguzia kero na usumbufu mkubwa wanaoupata sasa katika kupata baadhi ya huduma.
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa inategemea kumaliza zoezi la Usajili kwa mkoa wa Mara mwishoni mwa mwezi Februari, 2018 na kuendelea na hatua za uchakataji wa taarifa ili kuhakikisha wananchi wote wenye sifa waliosajiliwa mkoani Mara wanapatiwa Utambulisho wa Taifa kabla ya mwezi Desemba 2018.
 Wakazi wa kata ya Bukima Wilaya ya Musoma vijijini mkoani Mara,  wakiwa kwenye foleni wakisubiri kusajiliwa wakati wa zoezi la uandikishaji Vitambulisho vya Taifa.
 Mwenyekiti wa kijiji cha Bukima Ndg. Murungu Murungu akiwasaidia wananchi kujaza fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa wakati zoezi la Usajili likiendelea kwenye ofisi ya mtendaji kata ya Bukima.
 Afisa usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bi. Ohana Gerald akimsikiliza mmoja wa wananchi waliojitokeza kusajiliwa wakati wa zoezi la usajili  wananchi wa kata ya Bukima wilaya ya Musoma Vijijini mkoani Mara.
 Bw. Shukrani Kwikalya Mgane mkazi wa kata ya Bukima, akikamilisha hatua ya upigaji wa picha wakati wa zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa. Kulia ni afisa Usajili wa  Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bw. Jackson Paulo. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...