Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

MBUNGE wa Chalinze mkoani Pwani, Ridhiwan Kikwete(CCM)amesem amesikitishwa na kitendo cha watu kuingilia instagram yake na kisha kuandika maneno hajawahi na wala hawezi kuyasema.

Ridhawani ameiamba Michuzi Blogu kwa njia ya simu kuwa watu walioingilia instagram yake kabla ya kuandika maneno mabaya walizuia yeye asiingie. 

"Nimesikitishwa sana na hili jambo lililotokea leo.Watu wameingilia ukurasa wangu wa Instagram na kunizuia nisiingie kwenye account yangu. "Lakini jambo baya zaidi wanalolifanya ni kuandika vitu au maneno ambayo hata sijawahi na sitamani kuyasema.

"Nimeshangazwa sana na hili na sijui nia ya kufanya hivyo ni nini? Malengo yenu hamtafanikiwa,"amesema Ridhiwan. Amefafanua yeye yupo katika vikao vya halmashauri kupanga bajeti za Halmashauri yao ya Chalinze. 

Amesema hayo maneno na matukio hata hayajawahi tokea na anaomba utulivu wakati wataalamu wanafanya kazi ya kurudisha ukurasa huo mikononi mwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...