Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita aliyevaa koti la rangi ya dhambarau na miwani akipata maelezo juu ya matumizi ya kamera za barabarani kutoka kwa Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Geita, Mkaguzi wa Polisi Mark Thomas Masawe wakati wa ukaguzi wa mabanda ya maonyesho katika maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama mkoani humu.
ofisa wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) Hagai Ruben akitoa maelezo kuhusu ukataji wa leseni za usafirishaji kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani iliyofanyika kimkoa katika Mji Mdogo wa Katoro Geita.
Wataalam wa Jeshi la Zima Moto na Wokozi Mkoa wa Geita wakiwaeleza wajumbe wa Baraza la Usalama barabarani la Mkoa wa Geita juu ya matumizi mbalimbali ya mitungi yenye Gesi ya kuzima moto wakati wajumbe hao walipotembelea banda la kikosi hicho.
Emmanuel Chacha mtaalam kutoka Kampuni ya uchimbaji wa Dhahabu ya Geita (GGML) akitoa maelezo kuhusu matumizi ya vifaa vya wokozi katika maeneo ya migodi kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita na wajumbe wa baraza la Usalama barabarani .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...