Waziri wa Nchi, ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi)Selemani Jafo amewapongeza viongozi na watendaji wa wilaya na Halmashauri ya wilaya ya Mvomero kwa usimamizi wa Miradi ya maendeleo. 

Jafo aliyasema hayo alipokuwa ziarani wilayani huko ambapo alifanikiwa kutembelea ujenzi wa hospitali ya wilaya, shule ya kidato cha tano na sita ya kumbukumbu ya Sokoine, mradi wa ujenzi wa barabara ya lami, kituo cha mafunzo ya kilimo na mifugo, pamoja na mradi wa umwagiliaji. 

Katika ziara hiyo,Jafo ameagiza kuanza kwa utoaji wa huduma ya matibabu kwa wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya Mvomero ifikapo keshokutwa Desemba 13,mwaka huu wakati serikali ikitafuta fedha kwaajili ya ujenzi wa jengo la upasuaji, maabara, wodi ya watoto na majengo mengine ambayo yatagharibu zaidi ya sh.milioni 700 ambapo matarajio ni kupata fedha hizo na kukamilisha majengo hayo kabla mwezi Machi 2018. 

Pia Jafo ameagiza kuongezeka kwa kasi ya kukamilisha madarasa, bwalo la chakula na mabweni katika shule ya sekondari ya Sokoine Memorial kabla mwezi April 2018 ili shule hiyo iweze kupokea wanafunzi wa kidato cha tano hapo mwakani kwani serikali imepeleka fedha zote za ujenzi zaidi ya sh.billioni 1.6.

Aidha Jafo amewataka viongozi na watendaji kuendelea kushikamana ili kuwaletea wananchi maendeleo.

.Jengo la utawala na wagonjwa wa nje ya Hospitali ya Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akikagua shule ya kisasa ya Sokoine Memorial inayojengwa na serikali ya wilaya Mvomero.
.Jengo la kituo cha Mafunzo ya kilimo na mifugo kinachomaliziwa kujengwa wilayani Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akikagua ujenzi wa miundombinu wilayani Mvomero.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akiwa na viongozi wa mkoa na wilaya ya Mvomero wakati wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...