Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

KIKOSI cha Simba kimeanza kuandamwa na majeruhi baada ya John Bocco na Salim Mbonde kuungana na wachezaji wengine baada ya kuumia katika
mchezo wa ligi kuu Tanzania bara Jumapili iliyopita  dhidi ya Mtibwa Sugar na kushindwa kuendelea mchezo baada ya kupata majeraha.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba Hajji Manara amesema kuwa kwa sasa wachezaji wote wapo katika uangalizi wa daktari wa timu.

Amesema beki wa kati Salim Mbonde ambaye ni tegemeo katika safu ya ulinzi ya Simba atakuwa nje kwa wiki nne baada ya kuumia goti katika mchezo wao dhidi ya Mtibwa mwishoni mwa wiki iliyopita na atakosa michezo takribani minne  ikiwemo Njombe Mji, Yanga, lakini pia anaweza akakosa mechi nyingine mbili dhidi ya Tanzania Prisons na Mbeya City.

Ripoti ya madaktari inasema maumivu yake sio makubwa sana lakini anahitaji kukaa nje kwa ajili ya kutumia dawa lakini kama itakuwa vinginevyo basi tutawataarifu.


Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba Hajji Manara 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...