Kamati ya Miundombinu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania inaendelea na ziara ya kukagua ujenzi wa minara ya simu, ufikishaji na upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini na kwenye maeneo yasiyo na mvuto wa kibiashara ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata na kutumia huduma za mawasiliano kwenye maeneo mbali mbali nchini. Kamti hiyo imeendelea na ziara yake kwenye mikoa ya Dodoma na Tabora ili kujiridhisha na utendaji kazi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) wa kufikisha mawasiliano kwa wananchi.

Katika ziara hiyo, Mtendaji Mkuu wa UCSAF Eng. Peter Ulanga amesema kuwa Mfuko umetoa ruzuku kwa Kampuni ya simu ya TIGO kujenga mnara ili kufikisha huduma za mawasiliano kwa wananchi. Mfuko umetumia zaidi ya dola za marekani elfu arobaini na moja na mia tano (41,500) ambapo ni sawa na zaidi ya shilingi milioni 85 kuipatia kampuni ya TIGO kujenga mnara ambao sasa unahudumia zaidi wa wakazi 4,000 wa kijiji cha Mayamaya na vijiji vingine vya kata ya Zanka wilaya ya Bahi mkoani Dodoma ambapo walikuwa hawana huduma za mawasiliano na sasa wananufaika na uwepo wa huu mnara na wanapata huduma za mawasiliano. Mnara huu ulikamilika mwezi Machi mwaka jana na kuanza kutoa huduma ya mawasiiano kwa wananchi.

Naye mwakilishi wa kampuni ya simu ya TIGO mkoa wa Dodoma mhandisi Hassan Said Gimbo wa kampuni hiyo amewaeleza wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu waliofanya ziara ya kukagua ujenzi wa minara, ufikishaji na upatikanaji wa huduma za mawasiliano kuwa kampuni yao imekamilisha ujenzi wa mnara na sasa unatoa mawasiliano kwa wananchi. Pia ameongeza kuwa kampuni ya TIGO inafuatilia mara kwa mara kwenye eneo hilo na kuhakikisha kuwa mawasiliano yanapatikana. “Tunajitahidi kwa kiasi kikubwa kukarabati na kuhakikisha kuwa pale mawasiliano yanapopotea au kuwa hafifu tunafanya haraka kuyarudisha”, amesema mhandisi Gimbo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Prof. Norman Sigallla King (aliyesimama) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kizengi (hawapo pichani) kilichopo kata ya Kizengi wilaya ya Uyui mkoani Tabora baada ya kukagua ufikishaji na upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini wakati wa ziara ya Kamati hiyo. 
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Eng. Peter Ulanga(aliyesimama mbele) akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Bunge ya Miundombinu wakati wa ziara ya Kamati hiyo ya kukagua upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini kwenye kijiji cha Mayamaya kilichopo Kata ya Zanka wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.
Meneja wa Kampuni ya Simu ya TTCL Mkoa wa Tabora Bwana James Mlaguzi (wa kwanza kulia) akitoa taarifa kwa wajumbe wa Kamati hiyo wakati wa ziara yao ya kukagua upatikanaji wa huduma za mawasiliano viijini kwenye kijiji cha Kizengi kilichopo kata ya Kizengi wilaya ya Uyui mkoani Tabora.
Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Mussa Ntimizi akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Kizengi kilichopo kata ya Kizengi wilaya ya Uyui mkoani Tabora wakati wa ziara ya Kamati hiyo ya kukagua ufikishaji na upatikanaji wa huduma za mawasiliano vijijini.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...