Na Mwashumgi Tahir Maelezo Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Afya Zanzibar imewahakikishia wananchi kuwa Bohari kuu ya Dawa inadawa za kutosha za kuhudumia wagonjwa wanaofika kupata matibabu katika Mahospitali na vituo vya Afya.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman wakati alipofanya ziara katika Bohari kuu ya Dawa na kuangalia namna ya upatikanaj i wa dawa.
Amesema uwepo wa Dawa katika Bohari kuu ya dawa nikuonesha kuwa Serikali ina imani na wananchi wake kwa kuongeza Bajeti ya ununuzi wa dawa kwa asilimia mia moja ambapo upungufu upo kidogo kwenye dawa za wagonjwa wa akili ambap o Wizara iko mbioni kutatua tatizo hilo.
”‘Wananchi msininuwe dawa katika mahospitali na vituo vya Afya zipo za kutosha kwani Serikali imefanya jitihada kubwa ya kueneza dawa na kuzisambaza mahosptalini mote na vituo vya afya ambapo kama kutakuwa na upungufu wa dawa Wizara tutatoa taarifa maalum kwa wananchi wake”. Naibu Waziri huyo Alisisitiza.
Amewataka wafanyakazi wa Mahospitalini na Vituo vya Afya kuagiza dawa kwa wakati kwani kufanya hivyo kutasaidia kuondosha urasimu kwa wagonjwa ambao wanaokwenda kupata huduma ya matibabu na kuwambiwa dawa hakuna ambapo kuna dawa za kutosha katika Bohari ya dawa.
Kwa upande wa Mkurugenzi Bohari kuu ya Dawa Zahran Ali Hamad amesema kwa mujibu wa mahitaji ya dawa muhimu zinazotumika katika visiwa vya Unguja na Pemba dawa zipo za kutosha kwa kuwahudumia wananchi.
Amezitaja dawa hizo ni pamoja na za akinamama wanofika kujifungua,dawa za mpango wa uzazi, dawa ya kisukari na pressure na maradhi mengine na kuwasisitiza wahudumu wa afya kuagiza dawa kwa wakati.
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Bi. Harusi Said Suleiman akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Bohari kuu ya Dawa Zahran Ali Hamad alipotembea kuona dawa katika bohari hiyo, iliyopo Maruhubi Mjini Zanzibar.Picha na Makame Mshenga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...