Taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu wa Chama cha mchezo wa Baseball na Softball Tanzania ndugu Alpherio Nchimbi zinasema kwamba mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya yamekamilika kwa mfanikio makubwa ambapo zaidi ya washiriki 50 wamepata mafunzo hayo na kukabidhiwa vyeti vya kuhitimu. Mafunzo hayo yalitolewa na mwalimu mbobezi kutoka Japan ndugu Hiroki Iwasaki, yalianza tarehe 15 Julai na kukamilika jana Jumapili tarehe 16 Julai, 2017 yalikuwa ni ya siku nzima. "Intensive training program". Picha hizo zinaonyesha washiriki wakiwa viwanjani.
mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya
mafunzo kwa walimu pamoja na wachezaji wa Baseball Mkoani Mbeya
Baadhi ya washiriki 50 ambao wamepata mafunzo hayo na kukabidhiwa vyeti vya kuhitimu wakiwa na na mwalimu mbobezi kutoka Japan ndugu Hiroki Iwasaki
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...