Jubilee Insurance katika kuadhimisha miaka 80 ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo ya bima imezinduwa vyoo katika shule ya msingi Itiji iliyopo jijini Mbeya, vyoo hivyo vyenye jumla ya matundu 12 vilivyo jengwa na kampuni hiyo ya bima ya Jubilee Insurance na kuzinduliwa na Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania, Consoleta Cabone baada ya kuguswa na changamoto ya vyoo katika shule mbalimbali za msingi nchini.
Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania, Consoleta Cabone akizungumza baada ya kukabidhi vyoo hivyo, ambapo alisema "Naipongeza sana Jubilee Insurance kwa kujitoa kujenge vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Itiji, kwani ni jambo kubwa na linalo fanya na wacheche na badara ya kufanya sherehe kubwa katika maoteli kugawana kile kilicho baki kwenye bima na hatimae kurejeshwa kwa wananchi kwa kufanya mambo mema yenye baraka ikiwemo hili la ujenzi wa vyoo kwenye shule mbalimbali za msingi" pia Consoleta Cabone alitoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo yanayozungukwa na shule hiyo kulinda na kudhamini vyoo vilivyo jengwa na Jubilee Insurance.
Meneja wa Tawi la Jubilee Insurance kwa nyanda za juu kusini, Anne Qares akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi Meneja wa kanda nyanda za juu mamlaka ya bima Tanzania, Consoleta Cabone katika uzinduzi na ufunguzi wa vyoo vya wanafunzi wa shule ya msingi Itiji vyoo vilivyo jengwa na Jubilee Insurance.
Mkuu wa Shule ya msingi Itigi Mwl Lightness E. Makundi Akitoa shukran kwa Jubilee Insurance kwa ujenzi wa vyoo vya wanafunzi katika shule yake.
Mgeni rasmi akiwa katika zoezi la uzinduzi wa vyoo shule ya msingi Itiji iliyopo jijini mbeya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...