Katika kuelekea sikukuu ya Eid el-Fitri, E-FM Radio imetoa zawadi kwa wasikillizaji wake kama ilivyo tamaduni yake ya kutoa kwa jamii, ambapo wasikilizaji 10 kutoka jijini Dare s salaam waliofanikiwa kusikiliza redio na kujibu maswali kuhusu kampeni ya Kapu la sikukuu wameondoka na makapu yalioyo sheheni vitu mbalimbali ikiwemo vyakula muhimu kwa ajili ya sikukuu hiyo.
Tukio hilo limefanyika leo siku ya Jumamosi ya tarehe 24/06/2017 katika ofisi zao zilizopo Kawe – beach.DSTV nao waliongezea nakshi kwenye kapu kwa kuwazawadia washindi wa makapu ya sikukuu ving`amuzi vyao na kuwapa kifurush cha mwenzi moja bure. Zoezi hili litaendeshwa pia kwa washindi kutoka jijini Mwanza ambako EFM Radio inasikika kupitia masafa ya 91.3. washindi hao watajipatia zawadi zao za Kapu la sikukuu siku ya Jumapili tarehe 25/06/217 kwenye ofisi za DSTV Kenyata road Mwanza.
Washindi wa makapu katika picha ya pamoja wakisubiria kukabidhiwa makapu yao
Makapu ya Eid el-Fitri yakiwa yamesheheni vyakula mbalimbali
Washindi wa makapu katika picha ya pamoja wakisubiria kukabidhiwa makapu yao
Mwigizaji mashuhuri Riyama Ally ambaye ni balozi
wa Dstv akimkabidhi mshindi Benjamin n osha kapu lake la Eid el-Fitri’
Meneja wa vipindi wa Efm radio Dickson Mponela akimkabidhi
moja ya washindi Rebeca Lukule kapu lake la Eid Al Fitri
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...