Uongozi
wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), umesema utaendelea kuboresha
maslahi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo na kushughulikia tatizo la
upungufu wa wauguzi.
Mkurugenzi
Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru ameyasema hayo leo
katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, Tawi la Muhimbili ambayo
huadhimishwa Mei 12 kila mwaka. Kauli mbiu ya mwaka huu “ Wauguzi Mbiu
ya Kufikia Malengo Endelevu ya Milenia.”
Profesa
Museru amesema Serikali ipo bega kwa bega na hospitali hiyo katika
kupata ufumbuzi wa tatizo hilo. “Serikali imeahidi kutatua tatizo la
upungufu wa wauguzi katika siku chache zijazo,” amesema Profesa Museru.
Amesema
uongozi wa hospitali unashughulikia posho za wauguzi na pia
kuboresha
mazingira ya kazi ili wauguzi watoe huduma bora kwa wagonjwa.
“Pia uongozi wa muhimbili utaendelea kuboresha maslahi ya wafanyakazi ili wafanye kazi wa ufanisi,” amesema Profesa Museru.
Awali
mwakilishi wa wauguzi, Debora Bukuku alisoma risala ikielezea
changamoto mbalimbali zikiwamo mazingira magumu na hatarishi ya kazi na
pia kupitia risala hiyo waliomba wapatiwe posho za sare pamoja na
kuboreshewa maslahi mengine.
Katika
hatua nyingine, Mkurugenzi amewataka madaktari na wauguzi kuendelea
kuandika machapisho ambayo yanaeleza mafanikio na changamoto za utoaji
huduma zilizopo katika hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza na wauguzi leo katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani ambayo hufanyika Mei 12,kila mwaka.
Baadhi ya Wauguzi wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Museru katika maadhimisho hayo.
Baadhi ya Wauguzi wakirudia kiapo kwamba wataendelea kutoa huduma kwa wagonjwa kwa kuzingatia uadilifu.
Muuguzi wa Muhimbili, Furaha Tada akitoa mada kwenye maadhimisho hayo leo.
Wauguzi wakifuatilia mada iliyowasilishwa na mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...