Na Lydia Churi, Mahakama, Songea

Mahakama Kuu, Kanda ya Songea imefanikiwa kwa asilimia 100 kumaliza kesi zote zenye umri unaozidi miaka miwili Mahakamani.

Akitoa taarifa ya hali ya kesi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Songea, Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo Mhe. David Mrango alisema hadi kufikia Desemba 2016, Kanda yake ilikuwa na kesi 28 za jinai.

Alifafanua kuwa kesi za jinai zilizofunguliwa kati ya Januari na Mei mwaka huu zilikuwa 51na zilizomalizika na kutolewa hukumu ni 52 na zilizobaki kesi 27.

Kwa upande wa kesi za madai , Jaji Mrango alisema mpaka Desemba 2016, kulikuuwa na kesi 46 za madai kwenye Kanda yake , jumla ya kesi za madai zilizofunguliwa kati ya Januari na Mei 2017ni 42 na zilizosikilizwa na kutolewa hukumu ni 47 wakati zilizobaki ni kesi 41.

Alisema kati ya Januari na Mei, vikao viwili vya kesi za mauaji vilifanyika ambapo kesi 22 zilisikilizwa na 18 zilitolewa hukumu huku 2 zikibaki.

Kuhusu upatikana wa nakala za hukumu, Jaji Mfawidhi huyo alisema licha ya changamoto zilizopo, Kanda yake imekuwa ikitoa nakala za hukumu pamoja na mienendo ya kesi kwa wakati.

Mahakama kuu, Kanda ya Songea ni moja ya Kanda za Mahakama Kuu 13 nchini, Kanda hii ina jumla ya Majaji wawili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...