Ujenzi wa jengo la kuongozea ndege la Kiwanja cha ndege cha Mwanza, ukiendelea,
ambapo unatarajiwa kukamilika baadaye mwaka huu. Mnara huu umeelezwa utakuwa na
kiwango cha juu cha mawasiliano kwa nchi za Afrika Mashariki.
Jengo jipya la kuhifadhi mizigo la kiwanja cha ndege cha Mwanza, likiendelea na
ujenzi wake, jengo hilo linaukubwa wa mita za mraba 1500.
Mizigo ya mabaki ya samaki aina ya Sangara maarufu kama mabondo yakiwa kwenye
Kiwanja cha ndege cha Mwanza yakisubiri kusafirishwa nchini China kupitia Kiwanja cha ndege
cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), ambapo hutumika kutengeneza nyuzi zinazotumika
kushona wagonjwa kwenye hospitali.
Mwanzo wa ujenzi wa daraja la kuunganisha barabara ya kiungio cha ndege za
mizigo na barabara ya kutua na kuruka ndege, ambayo itawezesha ndege za mizigo kuelekea
kwenye jengo jipya la mizigo.
Afisa Usalama wa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza, Juma Nyamhanga (kushoto)
akimfafanulia mmoja wa abiria ujazo anaotakiwa kusafiri nao kwa chupa za mafuta na manukato
mbalimbali, kama alivyoishika pichani. Ujazo unaotakiwa kwa abiria kusafiri nao katika begi la
mkononi ni kuanzia ujazo wa 50-100, na ikizidi lazima uingie kwenye begi litakaloingia sehemu
ya mizigo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...