Na Veronica Simba – Dodoma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), umesitisha mkataba wa Mkandarasi Spencorn Services, aliyekuwa akitekeleza mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya pili kwa Mkoa wa Singida.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliyasema hayo hivi karibuni katika hafla ya uzinduzi wa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida, uliofanyika kijijini Mkwese, wilayani Manyoni.

Mhandisi Nyamo-Hanga alimweleza Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Mradi huo, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, ufanisi wa kazi wa Mkandarasi husika haukuwa mzuri hivyo kusababisha baadhi ya vijiji ambavyo vilipangwa kupelekewa umeme katika REA II, kutofikiwa na huduma hiyo.

“Tumechukua hatua za kinidhamu.Tumemsimamisha kazi na tutaleta wakandarasi wapya ambao wataendelea na kazi ya kusambaza umeme pale alipoishia.”

Aidha, Mkurugenzi Nyamo-Hanga alitoa shukrani kwa Serikali kwa ushirikiano na msaada ambao imekuwa ikitoa, ulioiwezesha REA kuendelea na zoezi la kuwafikishia umeme wananchi wa vijijini kwa mafanikio makubwa.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mwenye kipaza sauti) akiwatambulisha wafanyakazi wa Kampuni ya Nakuroi Investment Co. Ltd (waliochuchumaa), ambao watatekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu mkoani Singida.
Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Mkwese, wilayani Manyoni.
Moja ya vikundi vya ngoma kutoka Manyoni, kikitumbuiza katika hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Mkwese, wilayani Manyoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...