Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Machi, 2017 alikutana na Mawaziri
wa Nishati na Madini wa Serikali za Tanzania na Uganda Ikulu, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili Maendeleo
ya Mradi wa Bomba la
Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Chongoleani, Tanga
- Tanzania, hususan katika masuala ya kikodi yatakayotumika
katika mradi huo.
Mawaziri
hao ni pamoja na Waziri
wa Nishati na Maendeleo ya Madini Nchini Uganda, Mhandisi Irene Muloni pamoja
na ujumbe wake na Waziri wa Nishati na Madini Nchini Tanzania Profesa Sospeter Muhongo pamoja na
wataalam kutoka Serikali zote mbili.
Wajumbe wengine ni pamoja na Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. John Lukuvi, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, George Mcheche Masaju pamoja na Makampuni ya Uwekezaji ya Mkondo wa
Juu wa Ziwa Albert Nchini Uganda ya TOTAL, CNOOC na TULLOW.
Masuala
ya kikodi ni moja ya vipengele muhimu katika ukamilishwaji wa mkataba wa kimataifa
kati ya nchi ya Tanzania na Uganda.
Mbali
na kukaribisha washiriki wa mkutano huo, Mhe. Dkt. Magufuli alisisitiza ahadi yake na Rais wa Jamhuri ya
Uganda Mhe. Yoweri Museveni ya kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa
wakati.
Aidha,
Dkt. Magufuli aliagiza wawekezaji
kutekeleza mradi huo bila kuchelewa kwa maana
Serikali imeshaweka mazingira mazuri
ya utekelezaji wa mradi ikiwa ni pamoja na masuala ya usalama,
upatikanaji wa ardhi, kodi hivyo
kupunguza gharama za ujenzi Tanzania.
Pamoja na mambo mengine mawaziri, maafisa na
wataalam wa pande zote husika walikaa na kukubaliana kwamba, rasimu ya
makubaliano rasmi ya kuanza kwa mradi yawe yamekamilika na kuwa tayari katika
kipindi cha wiki mbili ili kuwezesha
Marais wa Tanzania na Uganda, kuweka jiwe la msingi kuashiria ujenzi wa kihistoria wa mradi huo wa bomba la mafuta kutoka Hoima
Nchini Uganda hadi Chongoleani, Tanga-Tanzania.
Mradi huu upo katika
hatua ya awali ya tahmini ya mazingira pamoja na kubaini maeneo mradi
utakapopita ili mradi kuweza kutekelezwa kwa kasi pindi utakapoanza.
Imetolewa na:-
Kitengo cha Mawasilino Serikalini
Wizara ya Nishati na Madini
Machi 29, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha pamoja cha Mawaziri wa Serikali za Tanzania na Uganda pamoja na wadau kuzungumzia mradi wa ujenzi wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga. PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...