Mkuu wa Wilaya ya Chemba Ndugu Simon Ezekiel Odunga akizungumza na wananchi wa kata ya Farkwa wakati wa uzinduzi wa zoezi la uthamini mali ili kupisha ujenzi wa bwawa la Farkwa.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma akiongozana na baadhi wa Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Wataalamu wa Halmashauri, Wataalamu kutoka Wizara ya Maji, Uvuvi na umwaguliaji, Wataalamu wa Bonde la Kati na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamezindua zoezi la uthamini wa mali za wananchi wa vijiji viwili vya Mombose na Bubutole watakaohama kupisha mradi mkubwa wa Ujenzi wa bwawa la Farkwa mkoani hapa.

Mradi wa bwawa la Farkwa ni mradi mkubwa ambao huenda ukawa ni mkubwa katika Ujenzi wa mabwawa makubwa kuliko yote barani Afrika. Mradi huu uliasisiwa na baba wa Taifa tangu mwaka 1970 utazinufaisha Wilaya za Bahi, Chemba, Chamwino na Dodoma Manispaa na utegemea kutumia pesa za Tanzania zaidi ya Tilioni 2.

Kufuatia umuhimu wa mradi huu na uwijio wa makao makuu ya nchi mkoani Dodoma, serikali imezamilia ifikapo mei mwaka huu zoezi la Uthamini wa mali za wananchi wanaohama kupisha mradi huu mkubwa katika Vijijini vya Mombose na Bubutole vilivyopo Wilayani Chemba pamoja na vijiji vinavyopitiwa na njia Kuu ya bomba linalopeleka Maji eneo la Kilimani mjini Dodoma liwe limekamilika tayari kwa kuwalipa wananchi ili Ujenzi wa bwawa uanze.

Ujenzi wa mradi huu unategemea kuchukua miaka mitatu 2017-2021 mpaka kukamilika kwake. Hivyo wananchi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa Wataalamu wa uthamini kwa kuwa wameusubiri mradi huu kwa zaidi ya miaka 47 na leo serikali imepata fedha ya kuutekeleza.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...