Na  Bashir  Yakub.

Yawezekana  katika  shughuli  zako  za  kila  siku unaingia  makubaliano  mbalimbali kama kuuza na  kununa  magari,  viwanja  na  nyumba, kutoa  huduma, kuajiri  na kuajiriwa, makubaliano  ya  vibarua, makubaliano  ya  kuagiza  mizigo  na  kupokea  mizigo, makubaliano  ya  kufanya  kazi   na  kulipwa  au  kulipwa baadae n.k. Makubaliano  yote  hayo  yaweza  kuwa  kwa  maandishi  au  kwa  mdomo. 

 Vyovyote  itakavyokuwa  swali  la kujiuliza  ni  kama  makubaliano  hayo  kwa  maandishi  au  kwa  mdomo  unaweza  kuyaita  mkataba.  Na  kama   yataitwa  mkataba  je  yanakubalika  kisheria.  Na je  sheria  inaweza  kukulinda  iwapo  limetokea  tatizo  lolote ?.

Tutahitaji  pia kujua  ikiwa  umedhulumiwa  katika  makubaliano   yawe  ya  maandishi  au  ya  mdomo   kama  inawezekana  kuchukua  hatua. Na je  ikiwa  makubaliano  hayo    sio  mkataba   ni  ipi  hadhi  yake  kisheria  na  yataitwaje. 

1.AINA   ZA   MAKUBALIANO.
Kuna  aina   kuu  mbili  za  makubaliano ambayo  yakikidhi  vigezo  yataitwa mkataba.  Kwanza  makubaliano  kwa  mdomo  na  pili  makubaliano  kwa  maandishi.

( a ) Makubaliano  kwa  mdomo   ni pale  unapokubaliana  na  mtu  katika  jambo  fulani  kwa  kuzungumza  tu.  Masharti,  vigezo  na  namna  ya  utekelezaji  wake  hufanyika  kwa  kuzungumza  tu. 

 Mpaka  makubaliano  yanakamilika  hakuna  popote  yanapokuwa  yameandikwa.  Jambo  la  msingi  hapa  ni  kuwa   aina  hii ya makubaliano  inakubalika  kabisa  kisheria . Ukweli  kuwa  hayakuandikwa  popote  katu  hauyabatilishi.

( b ) Makubaliano ya  maandishi  haya  ni  ya  kuandika.  Kila mlichokubaliana  kinawekwa  katika  maandishi  na  wahusika  wanasaini. Makubaliano  haya  nayo  yanakubalika  kisheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...