Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 17
Februari, 2017 amekutana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
(AfDB) anayeshughulikia masuala ya nishati Bw. Amadou Hott ambaye yupo hapa
nchini kwa mazungumzo na wataalamu na viongozi yenye lengo la kuboresha sekta
ya nishati hususan uzalishaji wa umeme.
Bw.
Amadou Hott amekuja nchini ikiwa ni utekelezaji wa mazungumzo yaliyofanywa kati
ya Mhe. Rais Magufuli na Rais wa AfDB Bw. Akinwumi Adesina Mjini Addis Ababa
nchini Ethiopia tarehe 31 Januari, 2017 ambapo viongozi hao walikubaliana
kuongeza ushirikiano kati ya AfDB na Tanzania katika maendeleo huku mkazo
ukielekezwa kupata majawabu ya kuongeza uzalishaji wa umeme na wa gharama nafuu.
Bw.
Amadou Hott ameelezea kuguswa na dhamira ya Mhe. Rais Magufuli juu ya kuongeza
uzalishaji wa umeme na wenye gharama nafuu kwa ajili ya kufanikisha mipango mbalimbali
ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa viwanda, na ameahidi kuwa Benki hiyo
itahakikisha dhamira hiyo inafanikiwa.
Kwa
Upande wake Mhe. Rais Magufuli amemhakikishia Bw. Amadou Hott kuwa Serikali ya
Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano wakati wowote itakapohitajika ili kufanikisha
dhamira hiyo.
Wakati huo huo,
Mhe. Rais Magufuli amekutana na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bharti Enterprises
inayomiliki kampuni ya simu ya Airtel Duniani Bw. Sunil Bharti Mittal ambapo
viongozi hao wamezungumzia utendaji kazi wa kampuni ya simu ya Airtel Tanzania
ambayo Serikali ya Tanzania inamiliki asilimia 40 ya hisa za kampuni hiyo.
Baada
ya mazungumzo hayo, Bw. Sunil Bharti Mittal ameelezea utayari wake wa kuingiza
kampuni ya Airtel Tanzania katika soko la hisa la Dar es Salaam ili Watanzania
wapate fursa ya kumiliki kampuni hiyo kwa kununua hisa.
Katika
hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hapa nchini Mhe. Jean Pierre Tshampanga
Mutamba Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais , IKULU
Dar
es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Amadou Hott aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
(AfDB) Amadou Hott Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Amadou Hott mara
baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) nchini
Jean Pierre Tshampanga Mutamba Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Balozi huyo wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) nchini Jean Pierre
Tshampanga Mutamba mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika
Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na kumkaribisha Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bharti
Enterrprise, Sunil Bharti Mittal aliyefika Ikulu kwa ajili ya
mazungumzo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bharti Enterrprise, Sunil Bharti Mittal
mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bharti Enterrprise, Sunil Bharti Mittal
Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...