Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Elimu na Ufundi Stadi Kanda ya Dar es Salaam VETA imetoa vifaa vya ufundi stadi vya thamani ya sh.milioni 11 katika atamizi ya Osarika Woodwork ikiwa ni sehemu ya kuendeleza atamizi hiyo kwa ujuzi na kufundisha vijana wengine wanaoenda kufanya mafunzo ya vitendo katika atamizi hiyo.

Akizungumza leo wakati hafla ya kukabidhi vifaa vya ufundi wa vitu vya samani katika atamizi ya Osarika Woodwork, Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam wa VETA, Habibu Bukko amesema kuwa vifaa hivyo walivyotoa kwa kikundi hicho kuongeza uzalishaji samani mbalimbali ikiwa ni pamoja kutoa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wanaotoka Veta.

Amesema vijana wa Osarika ni zao la VETA ambao wameweza kuunda kukundi na kusajili hivyo wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira lakini wameonyesha njia mpaka kuja kuongeza nguvu ya vifaa.

Bukko amesema vifaa hivyo ni mali kikundi cha Osarika wakivurugana vitu hivyo wanatakiwa kurudisha ili vikaweze kufanya kazi katika atamizi nyingine .

Aidha amesema kuwa VETA kuendeleza ni atamizi ni sehemu yao katika kuhakikisha atamizi zinaendelea katika kuzalisha ajira za vijana kutokana na mafunzo waliopata katika vyuo vya Ufundi.

Naye Mwakilishi wa Diwani wa Kata ya Tandika, Mwenyekiti wa Serikali Mtaa Mabatini ,Sharifu Jumbe amesema kuwa vijana wanatakiwa kujituma katika kufanya kazi na kuwataka wengine waende kupata mafunzo VETA.
 Sehemu ya misaada ya iliyotolewa na chuo cha VETA kanda ya Dar es Salaam leo katika kikundi cha Atamizi ya Orasika iliyopo Tandika jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuongeza nguvu kwa vijana ili kupunguza ongezeko la vijana wasio na ajira.
 Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mabatini-Tandika  ambaye ni Mgeni rasmi, Sharif Jumbe akimkabidhi moja ya kifaa cha Kukatia Mbao na Alminium mwanaatamizi ya Orasika-Tandika, David Mshilili jijini Dar es Salaam leo. Kulia aliyevaa Koti ni Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam, Habibu Bukko.
 Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mabatini-Tandika  ambaye ni Mgeni rasmi, Sharif Jumbe akimkabi baadhi ya vifaa vya ujenzi vijana wa atamizi ya Osarika jijini Dar es Salaam leo. 

 Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mabatini-Tandika  ambaye ni Mgeni rasmi, Sharif Jumbe, Viongozi wa chuo cha VETA, wanaatamizi ya Osarika wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanachi wa mtaa huo jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...