Kampuni ya Reli ya Tanzania (TRL) imefanya mabadiliko ya muda wa Treni ya Abiria kulekea mikoa ya Kigoma na Mwanza ambapo kuanzia tarehe 02 Agosti 2016 Treni itaanza kuondoka saa tisa(9) mchana badala ya saa 11 jioni muda wa sasa.

Mabadiliko hayo yametangazwa na Meneja Uhusiano wa TRL Midladjy Maez wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake leo Jijini Dar es Salaam.

Maez amesema kuwa mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa treni ya pili ya huduma za Jiji kutoka kituo Kikuu cha Reli cha Dar es Salaam kwenda Pugu ambayo itaanza kutoa huduma mapema siku ya Jumatatu ya tarehe 01/08/2016.

Aliongeza kuwa mabadiliko hayo yanahusu treni za abiria za huduma za kawaida zinazoondoka siku za Jumanne na Ijuma na kubainisha kuwa kwa upande wa huduma za treni ya Deluxe zitaendelea na muda wake wa kawaida.

“Uongozi umeamua kufanya mabadiliko haya kwa sababu za kiusalama zaidi kwani mabadiliko haya yataepusha muingiliano unaoweza kupelekea ajali na kuongeza kuwa kwa safari za kutoka Kigoma na Mwanza muda umebaki uleule”. Alisema Maez.

Meneja Uhusiano huyo aliongeza kuwa huduma za treni ya Jiji kwenda Pugu itakuwa na vituo 10 ambavyoa alivitaja kuwa ni pamoja na Pugu Stesheni, Gongo la Mboto,FFU Mombasa, Banana, (njia panda kwenda Stesheni), na karakata.

Vingine ni pamoja na Vingunguti Mbuzi,SS Bhakressa, Kamata na Kituo Kikuu cha reli Dar es Salaam.

Aliongeza kuwa huduma hiyo itakuwa na awamu mbili asubuhi na Alasiri ambapo treni ya kwanza itaondoka kituo cha Pugu saa 12 asubuhi na kuwasili kituo cha Dar es Salaam sa 12:55 asubuhi na kufanya safari tatu zitakazomalizika saa 05:15 asubuhi. 

Jioni kutakuwa na safari tatu ambapo treni itaondoka kituo cha Dar es Salaam saa 09:55 alasiri kwenda Pugu na kuwasili saa 10:50 jioni na safari ya mwisho kutoka Pugu kuja Kituo Kikuu cha Dar es Salaam saa 03:20 usiku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...