Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga   akiwa nje ya  jengo la  jumba la makumbusho la mkoa  wa  Iringa akiwa  katika mavazi  ya  Chifu wa  Wahehe


 Mratibu  wa mradi wa Fahari  Yetu Bw  Jimson  Sanga  akitoa maelezo kwa   Balozi Dr Mahiga kushoto  
WAZIRI  wa mambo  ya  nje  na ushirikiano  wa Afrika  Mashariki Balozi  Augustino Mahiga wa  nne  kushoto akiwa katika  vazi la  kichifu  wa Kihehe  na  viongozi  mbali mbali baada ya  kuzindua  jumba la makumbusho la mkoa  wa Iringa ,wa  kwanza  kushoto ni mkuu wa  wilaya ya  Iringa Bw Richard Kasesela na wa watano kutoka  kushoto ni mwenyekiti wa  wabunge wa  mkoa wa Iringa Bi  Ritta Kabati akifuatiwa na mkuu wa mkoa wa MOrogoro Bw
Kebwe Steven Kebwe
 Watenda kazi wa Makumbusho  hiyo  kupitia  mradi  wa Fahari yetu 
 Mratibu  wa mradi  wa Fahari Yetu  Bw  Jimso Sanga  kulia  akiagana na balozi Dr Mahiga 

 Na Matukiodaima Blog
Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga  amepongeza  jitihada za  chuo  kikuu  cha  Iringa kwa   kuwa karibu na serikali ya  mkoa  wa  Iringa  katika  uanzishwaji  wa   jumba la makumbusho la  mkoa (Iringa Boma) kwa  ajili ya  kuendeleza  kutunza tamaduni za  mkoa  wa Iringa na  kuongeza thamani ya  utalii katika  mkoa  na nyanda za juu kusini.
Asema  anaamini chuo  kikuu  cha  Iringa kinatekeleza  sera  ya  Taifa  ya ushirikiano  baina ya serikali  na  sekta  binafsi  katika kuwaletea  wananchi maendeleo endelevu.
Balozi Dr Mahiga  aliyasema  alitoa  pongezi  hizo  leo  wakati wa hafla  ya uzinduzi wa Jumba la Makumbusho la mkoa  wa Iringa mradi  unaoendeshwa na chuo  kikuu cha Iringa kupitia mradi  wa Fahari Yetu , hafla  zilizofanyika kwenye viwanja  vya bustani  ya  Manispaa ya  Iringa.
Alisema kuwa  makumbusho  hayo  ya  mkoa  wa Iringa  yatumike  kama chombo cha  kuchochea  maendeleo  kukuza  na kutunza tamaduni   za  mkoa   ili  kuleta maendele  ya  nchi  yetu  kwa  kuongeza thamani ya  utalii.
Pia  alisema  suala la  uhifadhi  na  ukuzaji  wa utamaduni  ni  suala  linalopewa uzito  mkubwa duniani  kote  hivyo   chuo kikuu  cha  Iringa  kwa  kushirikiana na serikali ya  mkoa  wa Iringa  wamebuni  jambo  jema  ambalo linapaswa kuendelezwa  kwa nguvu  zote. 
“Mataifa  mbali mbali anayojitambua  hutumia  fedha  na  raslimali  nyingi  sana kuhakikisha  jambo  hili  linafanikiwa  kwa  kiwango  cha  juu ….hivyo  basi wananchi wa  mkoa  wa Iringa  mnapaswa  kujivunia  na  kutumia fursa hii ya kupata  makumbusho ya  mkoa ndani ya jengo  hili  la  kihistoria  kuwa mmeletewa  nguvu  ya  kushikilia  tamaduni   na mila  zetu za makabila  ya nyanda  za  juu kusini zisiteteleke”.
Alisema  balozi  Dr  Mahiga  kuwa amefurahi sana   kuona  chuo  kikuu  cha Iringa  kinafanya  kazi  kwa  kushirikiana na  serikali ya  mkoa  kuendelea kuhifadhi tamaduni  za  wananchi  wa nyanda  za  juu  kusini.
“ Chuo  chetu  kikuu  cha  Iringa  kimekuwa   mbele   kwa   kutoa  kipaumbele katika  masuala ya  kukuza utalii  na utamaduni wa mtanzania  na hasa  kwa kutoa  wahitimu katika  sekta  hii ya utamaduni  nchini  ….walioandaliwa ili kulisaidia Taifa   katika Nyanja   hii ya utalii…. Hivyo  basi ni  wito  wangu  sasa kwenu kwamba  mzidi  kuboresha  mitaala yenu  mkiwa  ndio  chuo  cha  kwanza binafsi  nchini  ili  kuujenga zaidi mkoa  wa Iringa  katika  utunzaji wa utamaduni kwa  kufanya  tafiti zaidi hasa  katika eneo la utamaduni na  utalii ( Cultural Anthropology and Tourism) ili  kuipa  jamii na wadau wote uelewa  mpana  zaidi wa umuhimu  wa  kutunza na kukuza utamaduni wetu na utalii kwa ujumla kwa maendeleo ya jamii  zetu”
Katika  hatua  nyingine  waziri  Balozi Dr  Mahiga  ametumia   nafasi  hiyo ya uzinduzi wa makumbusho hayo  kumshukuru  Rais  Dr  John Magufuli  kwa kumteua kuwa  mbunge na baadae  kumteua  kuwa  mmoja kati ya  mawaziri wake  katika baraza lake la mawaziri na  kuwa  katika  uongozi  wake  kamwe hatamuangusha  Rais .

Alisema  kabla   ya  kuteuliwa  alikuwa mmoja kati ya  wana CCM ambao walijitokeza  kuomba  kuteuliwa na  chama kuwa mgombea  wa nafasi ya  ubunge japo  kura  hazikutosha   kutokana na  kuishi  nje ya  mkoa  wa  Iringa kwa  muda mwingi kama balozi  japo kurudi  kwake  serikalini ni  heshima  ya  wana Iringa na Taifa  kwa  ujumla ambayo Rais Dr Magufuli alimpa .



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...