Msanii wa kizazi kipya Vanessa Mdee (Wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na madansa wake wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Trust “Divas Only” lililofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dodoma. Tamasha hilo ni mahususi kwa utoaji elimu ya uzazi wa mpango kwa kina dada ambalo liliratibiwa na Shirika la DKT international.
 Msanii Vanessa Mdee (kushoto) akibadilishana mawazo na wafanyakazi mbalimbali wa Shirika la DKT International kabla ya kufungua rasmi Tamasha la Divas Only ambalo lilifanyika jijini Dodoma mwishoni mwa wiki. (Katikati) ni Meneja Masoko DKT International Sialouise Shayo.
 Kaimu meneja wa DKT International tawi la Dodoma Bi.Zena Mgoi akitoa elimu ya uzazi wa mpango kwa kina dada waliohudhuria uzinduzi wa Tamasha la “Divas Only” ambalo lililofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dodoma.

 Mwishoni mwa wiki TRUST wazindua mfululizo wa matamasha ya kusisimua ya Divas Only ambayo yalimshirikisha mwanadada na msanii wa muziki wa kizazi kipya Vanessa Mdee. 

Trust ni chapa ya njia za kisasa za uzazi wa mpango zenye kuaminika pamoja na bidhaa na huduma za maisha na urembo zinazotengenezwa na wanawake kwa ajili ya wanawake. 

Trust ipo ili kuhamasisha madiva wajipange kwa ajili ya baadaye,Madiva wa Trust wanataka kufanya maamuzi na kupanga kwa ajili ya mafanikio, Trust iko hapa kukusaidia wakati wa safari hii. 

Tulifurahia muda tuliopata kukaa na Vanesaa na Madiva wa Trust wa Dodoma, Kama wewe ni Diva wa Trust ama unataka kujua Trust inahusu nini, njoo ukutane na Madiva wa Trust wengine pamoja na Vanessa Mdee katika matamasha yetu mengine Mbeya Desemba 04 pale Sunset Hall, Soweto na Mwanza Desemba 13, Malaika Beach Resort. Huwezi kufika? Tafuta eneo lilipo Dodoma, Mbeya na Mwanza katika tovuti yetu (trustlife.co.tz) na ututembelee leo!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...