Na MatukiodaimaBlog

CHAMA Cha mapinduzi ( CCM) mkoa  wa Iringa  kimefuta matokeo ya kata tatu za jimbo la Kilolo matokeo yaliyokuwa yakimpa ushindi mkubwa mbunge anaemaliza muda wake Prof Peter Msola na kuagiza uchaguzi   huo  kurudiwa kesho

Matokeo hayo ambayo yamekataliwa na wagombea wote yanadaiwa kupachikwa katika  vituo vya kata hizo tatu japo hata hivyo hayana uhalisia ukilinganisha na idadi ya wanachama wa maeneo husika .

Katibu  wa CCM  mkoa  wa  Iringa Bw  Hassan Mtenga  alisema  kuwa  kutokana na dosari mbali mbali ambazo  zilijitokeza katika kata  hiyo  ambazo ni Nyalumbu , Lugalo na Uhambingeto  alisema  kilichoonyeshwa ni matokeo hayo kuwa  tofauti na matokeo  halisi ambayo mawakala wa  wagombea  walikuwa nayo na katika kata   hiyo makatibu matawi  na kata  wa CCM hahakuweza kupeleka matokeo kwa wakati kwa  msimamizi  mkuu wa  uchaguzi hadi  alipoyafuata na  kuona kasoro  hiyo .

Katibu   huyo  alisema karatasi  zilizoonyesha ushindi  wa mgombea  mmoja Prof Msolla zilikuwa ni tofauti na karatasi  halisi  zilizotolewa na chama   hivyo kutokana na utofauti  huo  wagombea  wengine  waliweza  kugomea matokeo hayo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Aibu.......ahahhahahah ndio magori ya mkono hayo ndani ya chama???+

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...