Wateja walioshinda katika bahati nasibu yetu na maeneo watokayo kwenye mabano ni pamoja na Simion Ngassa (Iringa), Sisco Haule, (Kigoma), Said M Mkinda (Dar es Salaam) na Phelis Nziku ambapo wote kila mmoja watakabidhiwa kiasi hicho cha pesa kutoka Bayport Financial Services. Naye Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Jehud Ngolo aliipongeza Bayport Financial Services kwa kuendelea kubuni mambo yanayoweza kuwapatia mwanga wateja na Watanzania kwa ujumla.

“Hii ni bahati nasibu nzuri na rahisi kuchezwa na kila mtu, maana haina vigezo zaidi ya mtu kuingia kwenye droo kama atakuwa amekopa tu, iwe kwenye mtandao wao au kufika katika tawi la ofisi yao yaliyoenea sehemu mbalimbali za Tanzania Bara,” alisema Ngolo, huku akiwataka Watanzania kuendelea kunufaika na huduma mbalimbali za Bayport. Huduma zinazotolewa na Bayport ni pamoja na mikopo ya fedha, mikopo ya bidhaa mbalimbali kama vile vifaa vya ujenzi, bodaboda, injini ya boti, pembejeo za kilimo, zikiwa ni miongoni mwa huduma zinazorahisisha maisha kwa Watanzania wote.
Zoezi la kuchezesha droo hiyo ya Kopa na Bayport likiendelea. Washindi wanne walijishindia Sh Milioni 1,000,000 kila mmoja.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Ngula Cheyo kushoto, akizungumza jambo kwenye heka heka ya droo ya kutafutwa washindi wanne wa shindano la Kopa na Bayport linaloendeshwa na Taasisi hiyo. Aliyefungwa kitambaa usoni ni Meneja wa Bayport Financial Services, Kanda ya Ziwa, Lugano Kasambala. Kulia ni Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Jehud Ngolo. Washindi hao wanne kila mmoja amejishindia Sh Milioni 1,000,000 baada ya kukopa kwenye taasisi hiyo ya kifedha nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...