Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifafanua jambo alipokuwa akihutubia umati wa watu waliofurika kumsikiliza  katika uwanja wa CCM Wilaya ya Sengerema ambapo aliwaambia wakazi hao Chama Cha Mapinduzi kitasimamia haki na misingi kwani ndio chama pekee kinachojali watu.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wapo kwenye ziara ya Kukagua na kuimarisha uhai wa chama,Kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010,katika Mikoa ya Kagera,Geita na sasa mkoani Mwanza.
 Mbunge wa Jimbo la Sengerema Ndugu William Ngeleja akihutubia wakazi wa Sengerema mjini kwenye mkutano wa hadhara ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni rasmi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Sengerema mjini kwenye uwanja wa CCM wilaya ambapo aliwaambia moja ya sababu kubwa ya kuporomoka kwa vyama vya upinzani nchini ni kutotaka kubadili viongozi na kubaki na viongozi wale wale ambao tangia 1995 mpaka leo wameshindwa kuleta mabadiliko kwenye vyama vyao na kuendelea kushindwa kwenye chaguzi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Nyamazugo kutoka kwa Mhandisi wa Maji mkoa wa Mwanza Ndugu Antony Sanga. Mradi huo mpaka kukamilika utakuwa na uwezo wa kutoa lita milioni 15 hivyo kuzidi mahitaji ya Sengerema ambayo ni lita milioni 8 kwa sasa,awamu ya kwanza ya mradi huo unategemewa kukamilika mwezi wa 8 mwaka huu na awamu nyingine inategemewa kukamilika mapema mwaka 2016.Pichani kushoto ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 kivuko kipya cha SUMAR III kitakachokuwa kinatoa huduma kati ya Sengerema na Mwanza kupitia feri ya Kamanga.
  Mbunge wa Jimbo la Sengerema Ndugu William Ngeleja akizungumza jambo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana (pichani kati) wakati wa uzinduzi wa kivuko kipya cha SUMAR III kitakachokuwa kinatoa huduma kati ya Sengerema na Mwanza kupitia feri ya Kamanga. 
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa kivuko kipya cha SUMAR III kitakachokuwa kinatoa huduma kati ya Sengerema na Mwanza.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...