Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar
Salum Mwalim akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika hivi karibuni
mjini Magu, mkoani Mwanza, ikiwa ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya
chama kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura na kujiandaa kupiga kura uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lisu akihutubia mkutano wa hadhara
uliofanyika hivi karibuni katika Uwanja wa Halmashauri, mjini Bariadi,
mkoani Simiyu hivi karibuni alipokuwa mkoani humo kwa ajili yakuzindua
mpango maalum uitwao 'Changia Chadema Kanda ya Serengeti ili Kushinda
Uchaguzi 2015' unaolenga kukusanya fedha kampeni za wagombea wa ubunge
na udiwani mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...