Ofisa Mkuu wa Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa (wa pili kutoka kushoto) akimkabidhi chetu cha uhitimu mmoja wa wahitimu wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru wakati wa mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika mjini Moshi, Kilimanjaro mwishoni mwa wiki. Ofisa huyo aliwakilisha wafanyakazi wa Vodacom kupitia Vodacom Foundation ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika kusaidia wasichana katika elimu ambapo kampuni hiyo pia ilitoa msaada wa mashine ya kutoa nakala na kuchapisha nyaraka kwa shule hiyo. Wengine ni Wajumbe wa Bodi ya Shule.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru Rosalia Tarimo (wa pili kutoka kushoto) akitoa hotuba yake wakati wa mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika mjini Moshi, Kilimanjaro mwishoni mwa wiki. Akifuatilia ni Ofisa Mkuu wa Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa (wa kwanza kushoto) ambaye pia alikuwa ni Mgeni Rasmi katika shughuli hiyo. Ofisa huyo aliwakilisha wafanyakazi wa Vodacom kupitia Vodacom Foundation ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika kusaidia wasichana katika elimu ambapo kampuni hiyo pia ilitoa msaada wa mashine ya kutoa nakala na kuchapisha nyaraka kwa shule hiyo. 
Ofisa Mkuu wa Uhusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Georgia Mutagahywa (wa tatu kutoka kushoto – mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Weruweru na wageni wengine waalikwa wakati wa mapokezi yake kama Mgeni Rasmi katika mahafali ya Kidato cha Sita ya shule hiyo yaliyofanyika mjini Moshi, Kilimanjaro mwishoni mwa wiki. Ofisa huyo aliwakilisha wafanyakazi wa Vodacom kupitia Vodacom Foundation ikiwa ni sehemu ya mchango wao katika kusaidia wasichana katika elimu ambapo kampuni hiyo pia ilitoa msaada wa mashine ya kutoa nakala na kuchapisha nyaraka kwa shule hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...