Mandhari ya nje ya Hoteli ya Kisasa ya Shangani Hotel Apartments iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego usiku jana mjini Mtwara. Pia ulizinduliwa Mgahawa wa kisasa ambapo wageni waalikwa walifaidi kula chakula cha usiku kilichopikwa na wapishi waliobobea kwa mapishi yenye vionjo vya kila aina.

Wageni wengine waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa hoteli hiyo itakayozidi kuongeza hadhi ya Mji wa Mtwara ni, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara, Seleman Mtalika na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Fatma S. Ally.Pia waliwepo wageni wengine kutoka taasisi mbalimbali pamoja na wafanyabishara. Hoteli hiyo inamilikiwa na Mkurugenzi Mtendaji Akida Zidikheri.
Akida Zidikheri (kushoto) mmiliki wa Shangani Hotel Apartments na . Said Aboud (kulia)pamoja na Mstahiki Mayor wa Manispaa ya Mtwara, Selemani Mtalika ndani ya mgahawa huo wa kisasa uliopo katika hoteli hiyo.
 Mmiliki wa Shangani Hotel Apartments, Akida Zidikheri wakiwa ndani ya moja ya Apartments pamoja naMkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego (kulia), na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara  Fatma S. Ally (kushoto).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...