Na   Bashir  Yakub.

Kifungu  cha 18  cha  Sheria  ya  Kanuni  za  adhabu  sura  ya  16  kimeeleza  hatua  ya  mtu  kujikinga  mwenyewe,  kumkinga  mwenzake  ,  mali  yake  mwenyewe  na  mali  ya  mwenzake. Kujikinga( defence)  maana  yake  ni  kujilinda  au  kujitetea  inapokwa  imekutokea  dharula   ya  kuvamiwa  na  mtu  au  watu  waovu. Uovu  ni  uovu  si  lazima  awe  mwizi .  Hata  mtu  asiyekuwa  mwizi  lakini  amekuvamia  kwa  nia  ovu iwe  nyumbani, kazini  au  sehemu  nyingine  yoyote  basi   ni  adui   unayepaswa  kujikinga  naye.

1.KUJIKINGA  NI  HAKI  YA  KILA  MTU.

Haki  ya  kujikinga  na  adui  si  tu  imeelezwa  katika  kifungu  nilichotaja  bali  pia  ni  haki  ya  msingi  ya  kikatiba.  Haki hii  pia  huingia  katika  zile  haki  ambazo  huitwa  haki  za  kuzaliwa ( in born right).  Haki  za  kuzaliwa  ni  zile  haki  ambazo  sio  lazima  ziwe  zimeandikwa  katika sheria  fulani  halafu  ndipo  mtu  azitekeleze .  Ni  haki  ambazo  hata  kama  hazikuandikwa  popote   mtu  ni  lazima  azipate  tu. Kwa  mfano  haki  ya  kula  au  ya  kuishi. 

Haihitaji  iwe  imeandikwa  popote  katika  katiba  au  penginepo  ili   uweze  kula  au kuishi.  Ni  kitu  ambacho  hutokea  moja  kwa  moja( automatic). Ni  kitu  ambacho  huandikwa  kama  haki  katika  sheria  lakini  hata  kisingeandikwa  ilikuwa  ni  lazima  kiwepo. Halikadhalika   ndivyo  ilivyo  katika  haki   ya  kujikinga ( defence) kwani  haihitaji kuwa  imeandikwa popote   kuwa  mtu  akikuvamia  kukudhuru   ujikinge  naye.  Inakuja  tu  moja  kwa  moja  mtu  akitaka  kukudhuru  ni  lazima  ujilinde  kwa  kutafuta  namna  ya  kujiepusha  naye. 

2. INARUHUSIWA  KUJIKINGA  HADI  KUUA.

Kifungu  cha  18c cha  sheria  hiyohiyo  ya  kanuni  za  adhabu   kinasema  kuwa   mtu  anaweza  kujikinga  mwenyewe, mali  yake  , kumkinga  mtu  mwingine, mali  ya  mtu mwingine  dhidi  ya  hatari   au  shambulio  mpaka  kufikia  hatua  ya  kuua  au  kusababaisha  madhara  makubwa  ya  kimwili. Madhara  makubwa  ya  kimwili  ni  pamoja  na  kukata  kiungo  cha  mtu  mfano  mguu,  mkono,  au  kusababnisha  madhara  mengine  kama  kusababisha  kidonda  kikubwa  na   hali  nyingine  zote zinazofanana  na  hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...