Dkt. Amosy Ephreim M'Koma, Mtanzania, Bingwa katika fani ya Upasuaji (Colon and Rectal Surgery). ametambuliwa na Jarida kubwa la watalaam mabingwa wa upasuaji duniani la "World Journal of Surgical Procedures" kutokana na  shughuli zake za utafiti (Surgical Sciences) katika Chuo Kikuu cha Vanderbilt University huko North Nashville, Tenesee. Dkt. M'Koma amekuwa taarifa kuu katik toleo la sasa la Jarida hilo (BOFYA HAPA) lenye bodi ya wahariri 275 ambao wote ni mabingwa wa upasuaji toka sehemu mbali mbali dunia.  Globu ya Jamii inampa hongera sana Dkt M'Koma kwa fanaka hiyo ambayo kupatikana kwake ni lazima uwe jembe kweli kweli kwenye fani hiyo.
Kumjua zaidi daktari pingwa 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Hongera sana Dkt M'Koma.

    ReplyDelete
  2. Michuzi safi kuwaweka wataalamu angalau balance iwepo, tunaona wasanii wamezidi sana kuwekwa, hongera sana profesa kwa kupeperusha bendera ya tanzania.

    ReplyDelete
  3. Hongera baba, lkn ingekuwa raha angekuwa anafanyia kazi zake hapa hapa tz

    ReplyDelete
  4. Hongera sana kwa nafasi hiyo. Leteni maendeleo nyumbani sasa jamani kwa elimu mulizopata huko nje. Leteni vifaa vya kisasa nyumbani na tujenge nasi hospitali bora tuache kwenda India na S.A. Tanzania tukiamua tunaweza kabisa

    ReplyDelete
  5. Loh! eti alete maendeleo nyumbani wapi Tanzania? Hell noooo! BIIg NO! unamkumbuka Dr. MAssawe wa Hospital ya Moyo? unamkumbuka Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar? na Unamkumbuka Dr. Muhongo? waje Nyumbani halafu yawatokee hayo? kama ningekuwa namjua ningemwambia akae huko huko!

    ReplyDelete
  6. Hongera Daktari tunakutakia mema unapoendelea kuchangia katika fani hii nchini na nje ya nchi. Endeleza kazi nzuri ikiwemo ya kupeperusha bendera ya wataalamu wa kitanzania..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...