Wasanii wa Goroa Tradition Dancing group wa Kata ya Qash Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, wakitoa burudani kwa wadau wa zao la ufuta, kwenye siku ya mkulima iliyofanyika katika kitongoji cha Maweni, Kata ya Endadosh Wilaya ya Babati Mkoani Manyara.
Afisa kilimo wa mradi wa ufuta wa shirika la Farm Africa, Tumaini Elibariki akimsikiliza Mtafiti wa Biosciences for Farming in Africa, kutoka London Uingereza, Claudia Canales kwenye siku ya mkulima iliyofanyika juzi katika kitongoji cha Maweni, Kata ya Endadosh Wilaya ya Babati Mkoani Manyara.
Mmoja kati ya wakulima wa mfano wa zao la ufuta, Edward Lemetei wa Kijiji cha Kakoi, Wilayani Babati, akipokea zawadi ya fedha kutoka kwa Afisa kilimo wa Mkoa wa Manyara, Coletha Shayo zilizotolewa na shirika la Farm Africa, katika siku ya mkulima kwenye kijiji cha Endadosh, kulia ni Afisa Mawasiliano wa Farm Africa, Goodness Mrema.
Mkulima wa zao la ufuta katika Kitongoji cha Maweni, Kijiji cha Endadosh, Kata ya Qash, Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, John Kunda, akiwaelezea Ofisa kilimo wa huo, Coletha Shayo na Ofisa kilimo wa mradi wa ufuta wa Shirika la Farm Africa, Tumaini Elibariki namna alivyoliendeleza shamba lake la ufuta.
Afisa kilimo wa mradi wa ufuta wa shirika la Farm Africa, Tumaini Elibariki akiwa ameshikilia kifaa cha kielekrtoniki (tablet) ambacho wakulima wengi wa zao la ufuta wamekuwa wakikitumia kwa ajili ya mafunzo ya kilimo na wakulima 397 wa Wilaya ya Babati Mkoani Manyara walinufaika na kilimo kupitia mafunzo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...