Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi
Wazazi na walezi wameshauriwa kuwapa watoto uji na ugali wa unga wa dona na siyo sembe kwakuwa unga wa dona una kiini cha mahindi ambacho kinakirutubisho kinachosaidia ukuaji na uwezo wa akili ya binadamu.
Ushauri huo umetolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete wakati akiongea kwa nyakati tofauti na viongozi wa Halmashauri kuu ya tawi ya Chama hicho katika matawi ya Mnazi Mmoja, Amani na Muungano yaliyopo katika kata ya Mingoyo wilaya ya Lindi mjini.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mke wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alisema siku hizi watu wengi wanapenda kutumia unga wa sembe ambao hauna virutubisho vyovyote katika mwili kwani unapokoboa mahindi kiini kinabaki katika pumba ambazo wanapewa wanyama na binadamu kukosa virutubisho vya muhimu katika miili yao.
“Watoto wetu wanatakiwa kupata lishe bora ambayo itawajenga akili zao, wasiwe na mambo mengi na kufanya zaidi ya kwenda shule na kusoma . Wakiwa shuleni watahitaji kunywa uji au kula chakula cha mchana hivyo basi ni muhimu kwa walezi kuchangia chakula cha mtoto kwakuwa mwanafunzi akishiba ataweza kusoma vizuri na kufaulu masomo yake .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...