Wasanii mahiri wanaounda kundi la THT wakiimba wimbo wa Malaria No More kabla ya mechi kuanza ya watani wa jadi Simba na Yanga.Wakati Vodacom Tanzania kushirikiana na Taasisi ya Malaria No More na THTwalipokuwa wakitangaza namba maalumu ambayo wateja wanaotumia huduma za kampuni hiyo wanaweza kuitumia kupata taarifa zinazohusiana na ugonjwa wa malaria. Ili mteja kuweza kupata taarifa hizo zinazohusisha jinsi ya kujikinga, tiba na masuala mengine mbalimbali ya Malaria anachopaswa mteja kufanya ni kujiunga kwa kutuma neno "Malaria" au "Mzinduka" kwenda nambari 15760 bila malipo.
Meneja Uhusiano wa Mambo ya nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim akitangaza namba maalumu ambayo wateja wanaotumia huduma za Vodacom wanaweza kuitumia kupata taarifa zinazohusiana na ugonjwa wa malaria. Ili mteja kuweza kupata taarifa hizo zinazohusisha jinsi ya kujikinga, tiba na masuala mengine mbalimbali ya Malaria anachopaswa mteja kufanya ni kujiunga kwa kutuma neno "Malaria" au "M zinduka" kwenda nambari 15760 bila malipo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...