Wasanii kutoka Tanzania wanatarajiwa kupamba maonesho makubwa mbalimbali nchini Ujerumani katika msimu wa joto.
Waliopata nafasi hiyo ni pamoja na kikundi maarufu cha ngoma ya Baikoko kutoka mkoani Tanga (picha ya juu).
Wengine ni mwanamuziki nguli wa reggae, Jhikoman & Afrikabisa band kutoka Bagamoyo, Pwani (picha ya chini) ambaye
amealikwa rasmi na Afrikative Organization
kushiriki onyesho kubwa la International Africa Festival Tubingen 2014 yanayoanza 17 mpaka 20 julai 2014 huko Tubingen, Ujerumani.
Wazee wa kazi Ngoma Africa band a.k.a. FFU Ughaibuni a.k.a. The Anunnaki Aliens (picha ya kati) kama kawaida yao watalishambulia jukwaa kuhakikisha washabiki wao hawapati usingizi.
si mchezo,naona ujerumani kumekucha
ReplyDeletewasanii wa bongo wanameamua kufanya kweli