Wasanii kutoka Tanzania wanatarajiwa kupamba maonesho makubwa mbalimbali nchini Ujerumani katika msimu wa joto. Waliopata nafasi hiyo ni pamoja na kikundi maarufu cha ngoma ya Baikoko kutoka mkoani Tanga (picha ya juu). 
 Wengine ni mwanamuziki nguli wa reggae, Jhikoman & Afrikabisa band kutoka Bagamoyo, Pwani (picha ya chini) ambaye amealikwa rasmi na Afrikative Organization kushiriki onyesho kubwa la International Africa Festival Tubingen 2014 yanayoanza 17 mpaka 20 julai 2014 huko Tubingen, Ujerumani. 
 Wazee wa kazi Ngoma Africa band a.k.a.  FFU Ughaibuni a.k.a. The  Anunnaki Aliens  (picha ya kati) kama kawaida yao watalishambulia jukwaa kuhakikisha washabiki wao hawapati usingizi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. si mchezo,naona ujerumani kumekucha
    wasanii wa bongo wanameamua kufanya kweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...